Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia bajeti hii ambayo kimsingi imebeba dhana ya Serikali ya Viwanda, naomba kuikumbusha Serikali mchakato wa viwanda 100 kila mkoa. Mkoa wa Katavi kutokana na kuendelea kuwa na changamoto za maji na umeme pamoja na masoko kutokana na miundombinu ya barabara kuwa kero kwa usafirishaji, naomba utekelezaji kwa kutatua kero hizi ili viwanda vilivyoanzishwa na vikundi mbalimbali ikiwemo viwanda vya alizeti, Manispaa ya Mpanda; viwanda vya mazao, mpunga na mahindi; viwanda vya maziwa (makanyagio); viwanda vya nyama, ukizingatia Mkoa wa Katavi kuna ufugaji wa kutosha viweze kuendelea. Hivyo, ni rai yangu kuomba Serikali hii kufungamanisha sekta ya ufugaji na viwanda ili dhana ya viwanda ifanikiwe.