Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, napenda kumshukuru Mungu kwa kupata nafasi ya kuchangia hoja iliyopo mbeye yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, wafanyabiashara wengi wanalalamikia suala zima la ushuru. Wafanyabiashara wanapofikia mpakani kibali cha kuingiza bidhaa nchini imekuwa ni kero. Kuna kulipia ushuru wa TFDA, VAT na tozo nyingine nyingi. Mfano unaingiza pipi, biskuti, tende na kadhalika unatakiwa ulipie Sh.800,000 kwa kila bidhaa, mfano hizo bidhaa tatu itabidi ulipie Sh.2,400,000 kwa miaka mitano. Je, mfanyabiashara ambaye mtaji wake ni mdogo Serikali haioni kuwa inamkandamiza mfanyabiashara huyo?

Mheshimiwa Naibu Spika, utakuta magari ya mizigo, mfano Kenya kuja Tanzania ni mengi kuliko Tanzania kwenda Kenya kwa vile kuingiza bidhaa Kenya kuna unafuu wa ushuru. Nashauri kama itawezekana masharti yalegezwe TFDA angalau mzigo utozwe kodi 1% kila mzigo unapoingizwa. Pia Soko la Afrika Mashariki wawe na kituo kimoja cha Bureau of Standards ambapo bidhaa zao zinalipwa ushuru baada ya kupimwa badala ya kazi hii kufanywa na TFDA.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna magari maalum ya kubeba kemikali lakini magari haya yanawaumiza wafanyabiashara wadogo kutokana na tozo ilivyo kubwa. Mfano, kuna wafanyabiashara wadogowadogo ambao wanaingiza nchini office glue, inabidi mfanyabiashara awe na gari maalum lililosajiliwa hata kama ana carton 50 za office glue inahesabika kuwa ni kemikali, huwezi kubeba carton 50 katika gari la tani 10.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri uwepo utaratibu wa kusajili magari hata kuanzia tani moja. Hii ya kusajili tani 10 imelenga kwa wafanyabiashara wakubwa na kuwaacha wafanyabiashara wadogo kuendelea kubaki maskini. Naiomba Serikali iangalie suala hili la magari ya kubeba kemikali.