Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, kufanya ziara/kongamano la wawekezaji na wafanyabiashara Mafinga. Wakati tunaelekea uchumi wa viwanda, Mafinga tumepiga hatua kubwa hasa katika suala zima la mazao ya misitu. Hata hivyo, tuna changamoto nyingi sana kuanzia masuala ya Regulatory Authorities lakini pia kuna fursa kutoka TIB, TADB na kadhalika. Nimeomba mwaka wa nne sasa Serikali (Wizara) kwa kushirikiana na Serikali ya Mkoa, Wilaya na Halmashauri tufanye kongamano Mafinga.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la PVOC, binafsi baada ya kuhudhuria semina ya TANTRADE ambapo TBS na WMA walitoa mada kati ya hizo niliuliza suala la PVOC ambalo kwangu mimi naona ni kuwanufaisha watu kati (the so called agents). Maana kazi kubwa inafanywa na TBS za nchi husika, mfano ukitoa mzigo China lazima pawepo TBS ya kule itoe certificate lakini tena mtu analipa dola 800 ili upate COC, inapotea bure. Afadhali ingelipwa hapa, kwa sababu pamoja na yote hayo bidhaa ambazo ni fake na substandard zinaingia nchini. Makusudio yangu ni kushika shilingi hasa ikiwa hapatatolewa maelezo ya kutosha.