Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia katika hotuba hii. Naomba nianze moja kwa moja kwa sababu ya muda, katika kuzungumzia masuala mawili muhimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni suala zima la uwezeshwaji au mazingira bora ya uwekezaji pamoja na kufanya biashara. Haya maeneo ni muhimu sana na ndiyo hasa yanabeba uzito mzima wa jinsi ambavyo maendeleo ya biashara au viwanda nchini kwetu yatakwenda. Kwa bahati mbaya sana, Wizara yenyewe inapata bajeti ndogo mno kiasi kwamba hata ile kazi ya kuandaa ule uwezeshwaji inakuwa siyo rahisi kiasi hicho. Tumejionea jinsi ambavyo bajeti iliyopangwa na bajeti iliyotolewa ni ndogo sana katika matumizi ya kawaida na hata ya maendeleo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hayo, kuna suala zima la kuweka mazingira bora ya uwekezaji katika viwanda vyetu. Nataka kukumbusha Serikali kuwa mwaka 2010 task force iliundwa ya Wizara nane kwa ajili ya kutengeneza roadmap ya kuweka utaratibu ambao utarahisisha uwekezaji na vilevile kufanya biashara. Task force ile ilikuja na mapendekezo mazuri sana na chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kulikuwa kuna uratibu sasa wa jinsi gani ya kutekeleza yale mapendekezo yaliyotokana na ile roadmap ya kwanza ambayo ilikuwa inalenga ku-improve uncompetitiveness ya uendheshaji wa shughuli zetu nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa sielewi ile ilifikia wapi kwa sababu mwaka jana tena tulikuja na blue print na vyote vinatokana na taarifa zinazotoka nje kuonyesha kuwa sisi ranking yetu inazidi kudorora. Sasa hii blue print haikuwa tofauti sana na ile roadmap ya kwanza lakini pamoja na hayo yote bado hatuoni jinsi gani ambavyo tuna mwelekeo unaotutoa hapa tulipo ambapo bado hatujakuwa na mwelekeo mzuri wa jinsi ya kuanzisha viwanda na kuviimarisha. Tunaona kabisa na ni ukweli usiopingika kuwa biashara zinadorora na nyingine zinafungwa, wawekezaji hawana amani kwa kifupi naweza kusema hivyo, wawekezaji waliopo na wale ambao wanataka kuja bado hawajakuwa na amani.

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu inasemekana ni ya amani na utulivu lakini kiuchumi na kibiashara hakuna huo utulivu wala amani. Nasema hivyo kwa sababu ya jinsi ambavyo shughuli zinaendeshwa; kwanza maamuzi yanachelewa sana kufanyika na hii tunazungumzia tangu vibali vinapoombwa mpaka proposal zinapoletwa na wawekezaji wanaotaka kuja kuwekeza mpaka inapofikia kuwa sasa wanaanza kufanya shughuli zao au wanaamua kuondoka. Huu muda ni mrefu mno kwa mtu ambaye anataka kuja kufanya biashara. Tunajua kabisa katika biashara muda mali, hawezi mwekezaji kuja kukaa miezi mitatu hotelini hapa anangojea decisions na wakati tumesema tuna TIC ambayo ni one stop center; hiyo one stop center kwa nini ichukue miezi mitatu kuamua jambo la mwekezaji anapokuja nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hayo, kuna mambo madogo madogo mengi ambayo yanaleta tatizo; yamezungumzwa humu ndani masuala ya permit, ajira na hata mikopo kwa ajili ya wawekezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nizungumzie suala ambayo yamejitokeza katika ranking ya hivi karibuni ambayo ilipata kwa ajili ya Serikali yetu. tumefanya vibaya sana kwenye masuala ya cross border trade ambayo sisi tuna advantage kubwa sana; tuna fursa kubwa sana katika biashara ya mipakani kwa sababu tuna mipaka mingi sana Tanzania na wazalishaji wadogo wadogo wengi na hasa wakiwa akinamama ndiyo wenye nafasi kubwa sana ya kufanya hiyo, lakini tumefanya vibaya. Tuna fursa kubwa ya kufanya biashara sisi na nchi nyingi zinazotuzunguka pamoja na Afrika ya Kati, lakini tumekwama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna matatizo vilevile ya masuala ya kodi na hii inaletwa na biashara kuwa siyo nzuri sana kwa hiyo hata kodi kukusanya inakuwa vigumu. Tunajikuta tunazunguka katika vicious circle ya kutokuwa na mikakati mizuri kwa sababu tu ya jinsi ambavyo tunaendesha hizi shughuli zetu sisi wenyewe. Matatizo yote tuliyonayo ni…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)