Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuchangia mchana huu. Kwanza kabia naomba niweke record sawa. Naona kuna baadhi ya wenzetu hawaelewi hii certificate of original inatolewaje? Ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge, cerificate of original anapewa exporter. Akishapewa exporter, yeye anaweza akawa anapeleka sehemu tatu tofauti. Kwa hiyo, sehemu zinazokwenda, zinaenda nakala, certificate of original anabakinayo exporter. Kwa hiyo, ninaungana mkono na wenzangu waliotangulia, hasa Mheshimiwa Turky kwamba, siyo sahihi TRA kudai certificate of original kwa sababu certificate of original ni mali ya exporter. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hilo nilikuwa napenda nichangie sehemu mbili ambazo nilikuwa nimejipanga nichangie. Suala la kwanza ni suala la wakala wa vipimo. Wote tunajua tatizo la vipimo lilivyo. Kwenye taarifa ya Mheshimiwa Waziri amesema kwamba anategemea kuajiri watu 153. Katika kero ambayo inaendelea katika maeneo mengi hasa ya nchi yetu ni suala la vipimo. Vipimo vinatumika kwa wakulima, madukani na kila mahali, hata barabarani magari yanapimwa kwa kutumia vipimo. Vile vipimo vimetengenezwa na vyuma na ofisi za vipimo ziko mikoani tu. Kwa hiyo, wanakagua maeneo mengi hivyo vipimo kwa mwaka mara moja. Kwa hiyo, utakuta mara nyingi wanaotumia vipimo wanakuwa wanawapunja wateja wao kwa ajili ya vipimo ambavyo wanavitumia.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba sana Wizara mjipange kufungua ofisi kwenye wilaya ili wale watumishi wa vipimo upande wa wilayani waende kukagua mizani ile mara kwa mara. Kwa sasa watu wanaotumia vipimo wanapata tabu sana, wakitaka huduma ya watumishi wa vipimo lazima mtu aende mikoani, hasa watu wa mafuta shida hiyo wanayo, mizani mingi shida hiyo wanayo ndiyo maana wakulima wengi wanalalamika kwamba wanapunjwa katika vipimo vyao ambavyo wanavitumia wafanyabiashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ambalo napenda nilichangie ni suala la mfumo wa stakabadhi ghalani. Mfumo huu upo kwa mujibu wa sharia, lakini kanuni zimeleta matatizo mengi ambayo yamesababisha watumiaji wa mfumo ule kuwa tofauti. Kwa mfano, sasa hivi limezuka janga, hawa wanaotumia mfumo wa stakabadhi ghalani hasa wakulima na vyama vya ushirika kupunjwa mazao yao yanapopotea kwenye maghala makuu, lakini hatua yoyote inayochukuliwa kutoka kwenye Serikali au kwa mfumo wa stakabadhi ghalani. Kwa hiyo, naomba Sheria ya mfumo wa Stakabadhi Ghalani irekebishwe ili kuhakikisha kwamba inaweza kumlinda mkulima au mtumiaji wa mfumo wa stakabadhi ghalani aweze kupata haki yake ya mapunjo ambayo yanatokana na matumizi ya mfumo wa stakabadhi ghalani.

Mheshimiwa Naibu Spika, tukiangalia mfano halisi uliopo kwenye Sekta ya Korosho, sasa hivi korosho zipo maghalani na tunategemea kwenye mazao mengine tutumie mfumo wa stakabadhi ghalani, sehemu ya kuhifadhi yale mazao hakuna. Naomba, nadhani Serikali jambo la kwanza kulitilia maanani lingekuwa ni suala la kuongeza maghala katika maeneo yetu ambayo yanazalisha mazao, bila kuwa na maghala, mfumo wa stakabadhi ghalani hauwezi kufanya kazi kama wanavyosema wenyewe mfumo wa stakabadhi ghalani. Kwa hiyo, naomba sana Serikali kwa ku-rescue situation iliyopo sasa kwa upande wa maeneo ya kusini, basi ichukue hatua za haraka ili kuongeza maghala katika maeneo mbalimbali ili korosho au mazao yaweze kuhifadhiwa kama yanavyotarajiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hiyo, kuna risk kubwa kwa upande wa ma-warehouse operator ambao wanafanya shughuli zile, wanaingiliwa sana na Serikali tofauti na sheria inavyohitaji kuhusu huu mfumo wa stakabadhi ghalani. Sasa hivi wengi ma-warehouse operator wanaogopa kufanya kazi ile kwa sababu muda/wakati wowote wanaweza kuwekwa ndani bila ya utaratibu, jambo ambalo linakatisha tamaa watumiaji wa mfumo wa stakabadhi ghalani. Hii inapoteza haki yao ya msingi ambayo ipo katika mfumo wa stakabadhi ghalani. Naomba sana Serikali iangalie hii sheria, iangalie upungufu wote uliopo kwenye mfumo wa stakabadhi ghalani urekebishwe ili wadau wa mfumo wa stakabadhi ghalani uweze kupata haki yao kwa mujibu wa sheria.

Mheshimiwa Naibu Spika, hayo ndiyo nilikuwa napenda nichangie. Ahsante sana kwa kunipa nafasi. (Makofi)