Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kupata nafasi hii. Pia nawatakia kheri Waislamu wote wanaofunga Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nitakwenda kwenye viwanda, kweli Serikali ya Awamu ya Tano imejenga viwanda vingi lakini viwanda hivi kama havikuangaliwa vizuri basi vitakufa haraka sana. Ni lazima viwe na watu wenye ujuzi wa kuviendesha viwanda hivi.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia wawe na viwanda vya malighafi kwa sababu malighafi nyingi inaagiziwa kutoka nje ya nchi na kuleta hasara kwa Taifa. Kwa hivyo, ni lazima viwanda vijengwe hapa ili kupunguza gharama na kuipatia mapato Serikali hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi Mwenyezi Mungu katika nchi yetu ametujalia utajiri mkubwa yakiwemo maziwa na bahari. Katika nchi yetu tunazungukwa na bahari katika ukanda wa Pwani wa Dar es Salaam, Tanga, Lindi, Zanzibar, Pemba na sehemu nyingine lakini hakuna viwanda vya kuchakata samaki, tunakosesha Tanzania kupata mapato. Kwa hivyo, Serikali ijipange kujenga viwanda vya minofu ya samaki. Tunawaachia Wachina wanakuja na meli zao, wanavua samaki wanaondoka nao sisi tupo tunaangalia. Kwa hivyo, Serikali ijipange kujenga viwanda hivyo hata Zanzibar na Pemba. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaambiwa kuwa Zanzibar siyo nchi, Tanzania ni Taifa moja lakini kinachosikitisha bidhaa zinazotoka Zanzibar kuja Tanzania Bara hawapewi vibali. Tuna sukari, maji ya drip na maziwa lakini haviruhusiwi kuingia Tanzania Bara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, cha kushangaza Tanzania Bara inaleta vitu Zanzibar mfano bia, sigara, soda na vitu vinginevyo, kwa nini na wakati ni nchi moja? Kwa nini na sisi hatufaidiki? Nchi moja itakuwa tukiwa Zanzibar lakini tukiwa Bara ni nchi mbili? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine, mfano wa magari. Gari linapotoka Tanzania Bara tunalipa ushuru, lakini linapoingia Zanzibar unalipa tena ushuru mara mbili. Ni kwa nini ilipe ushuru mara mbili? Hili ni tatizo.

MBUNGE FULANI: Na ni nchi moja.

MHE. MGENI JADI KADIKA: …na ni nchi moja. Kwa nini tufanye hivyo? Kuna nini? Naomba basi, kama ni nchi moja, basi isiwe tunalipishana ushuru mara mbili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni kuhusu wafanyabiashara. Kwa kweli, Wafanyabiashara tunawarudisha nyuma au Serikali inawarudisha nyuma kwa sababu kodi inayotozwa ni kubwa mno. Mfanyabiashara anapewa mahesabu anaambiwa miaka mitatu hujalipa; sijui hivi, kuna hili, kuna hili, inapigwa thamani ya kupewa mfanyabiashara wakati ile biashara yake aliyonayo kwenye duka haitoshi. Ile biashara yake yote ikipigiwa thamani haitoshi, tunampeleka wapi mfanyabiashara huyu? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana wafanyabisahara wengi wamefunga maduka yao, wafanyabiashara wengi wanarudisha leseni. Je, tunakwenda wapi? Tunakwenda wapi? Serikali hii hatuko masikini, tuna utajiri wa kutosha, kwa nini tuwabane wafanyabiashara wao tu? (Makofi)