Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupata nafasi hii ili niweze kuchangia katika hotuba hii ya Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara. Hotuba hii ukiisoma ni nzuri na nampongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu wake kwa kuandaa bajeti hii na hotuba hii ambayo kwa kweli inaakisi kile ambacho wanadhani wanaweza kukifanya mwaka ujao wa fedha. Naomba nianze kwanza kwa masikitiko yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Watanzania na hasa na sisi Waheshimiwa Wabunge, tusipokubaliana kwanza kubadilisha mawazo yetu kwa kuthamini kwamba biashara au public sector ndiyo kiini na kitovu cha ajira za Watanzania. Ndicho ambacho kinaweza kukuza uchumi wa nchi hii, short of that hatuwezi kutoka hapa tulipo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumezoea kuitana majina; fisadi, mwizi, ukimuona mtu anafanya hivi huyu ni mwizi. Hebu jiulize; kama ameweza kuiba na akawekeza hapa nchini, wizi wake uko wapi? Kwa sababu tunavunjana moyo Watanzania, sisi tukiona mtu ametajirika anaitwa fisadi, anakuwa mwizi, haya maneno hayatusaidii kutujenga Watanzania na naomba sana tufanye a total mindset transformation, tusipofanya hivyo Watanzania itabaki ni hadithi tu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais ameingia na kuali mbiu sahihi kabisa, hajaianza leo, ameakisi watangulizi wake. Tunataka Tanzania ya viwanda, unapataje viwanda? Lazima kuwe na backward and forward linkages. Hayo unayapata kama Watanzana wameshirikishwa vizuri, lakini leo hii Private Sector ina matatizo chungu nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii kuanzisha biashara Tanzania ni kama mzigo, utatozwa kodi kwenye mtaji ambao unataka uwekeze. Sasa how can you invest on your capital? Tuangalie tu, hiyo capital unakwenda kukopa benki, kabla hujaitumia unatandikwa kodi karibu 42, sasa unakwenda wapi. Sasa ni mambo ambayo sisi kama Watanzania lazima tubadilike. Tusipobadilika itakuwa ni hadithi na ngonjera, tunabaki kila siku tunasema sisi tumelogwa, hakuna aliyetuloga, ni mawazo yetu yamelogana yenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia vibali vya kufanya kazi, unajua uchumi wowote wa nchi ni mixture, unaweza uka-borrow technology, uka-borrow capital kutoka kwa watu mbalmbali uka-invest. Kama huna technology hiyo unai-borrow from outside, lakini sisi hapa tunaona hata wageni ni tatizo, sasa unajengaje uchumi wa kwako peke yako? Tunaomba sana katika hili tubadilike. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo ambayo ukiyaangalia, Mheshmiwa Waziri amezungumza kwenye hotuba yake, non-tariff barriers, wamepunguza kutoka 62 mpaka 47, this is very good, lakini leo hii hata kusafirisha mzigo tu ukienda kilometa kadhaa mizani unaambiwa faulisha, mara fanya kitu gani, una waste a lot of time barabarani kabla ya kufikisha mzigo unakokwenda; hivi ndivyo vinavyoleta uchachu katika kufanya biashara hapa nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu vilevile kuna taasisi ambazo zinapaswa kuwa harmonized. Namshkukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuanzisha Wizara ya Uwekezaji, nampongeza sana, angalau sasa, tena kaiweka chini ya Waziri Mkuu, kwamba angalau Waziri Mkuu moja kwa moja anawajibika katika suala la uwekezaji kupitia Waziri ambaye amepewa mamlaka hayo. Hii itasadia kutufanya Watanzania tuthamini namna ya uwekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi Mheshimiwa Waziri Mkuu amepokea watalii kule Arusha, it’s a business, utalii is a business. Sasa sisi hapa unaangalia kwamba tuna vituo vingi sana, lakini tunalia kwamba hatuna wawekezaji, watakujaje hatujaweka mazingira mazuri hapa kwetu? Naomba Bunge hili litumike kuhakikisha kwamba tunaweka utaratibu mzuri wa ufanyaji biashara, bila hivyo itabaki ni ngonjera. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona na naomba nim- quote Mheshimiwa Naibu Waziri wa Fedha, alisema kwamba biashara nyingi zinafungwa, lakini nyingi zinafunguliwa, sio kweli. Biashara nyingi zinafungwa sasa hivi na watu wana- scale down, tunapaswa kama Serikali, kama nchi, tujitathmini upya, why, bila kufanya vile unapataje hiyo kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Watanzania tusiseme kwa sababu watu pengine wanapiga makofi huku, hoja ni kwamba lazima tutoke hapa tulipo, tufike mahali pazuri. Kwa hiyo kwa sababu unajua wakati mwingine tusipoambizana ukweli hatuwezi kusonga mbele. Nimwombe sana Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Rais amempa nafasi hii, hebu atumie nafasi hii sasa kuweza kufanya mabadiliko makubwa ya kiuchumi ili Tanzania tusonge mbele, hatuwezi kila wakati kuwa tunalia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii ukienda by statistics makusanyo ya kodi ya TRA yanazidi kushuka, wakatae wasikatae ukweli ndiyo huo, lakini yanashuka kwa sababu gani? Lazima tuchochee tupate biashara nyingi, unapata kodi hii kutoka kwenye biashara, uta-tax wapi kama hakuna biashara, niombe sana. Marehemu Dkt. Mengi ni mmoja wa Watanzania ambaye alijitahidi sana kufanya biashara mbalimbali, nikiuliza leo hii hapa Tanzania baada ya Dkt. Mengi kufariki, wangapi akina Mengi saa hizi, wangapi? Tukikaa hapa, ukiona hivi unasema wengine hapa Tanzania wapo, lakini unakuta wana passports zaidi ya moja au mbili, unakuta yeye peke yake akifanya biashara asilimia 75 anapeleka nje, lakini ukiwa kama mimi namna hii au wewe au ndugu yangu hapa Mr. White, akipata hela yake hapa ataoa mwanamke hapa, atawekeza hapahapa, hela inazunguka hapa hapa. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona niseme haya kwa sababu naumia kuona kwamba this is my country, lakini kila siku tunalalamika, tunamlalamikia nani? Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara, tusaidie. Hata hivyo, lazima wasomane na wenzake, hawezi akafanya kazi in isolation, wasiposomana haiwezkani, naomba apate support kwa Mawaziri wenzake ili tuwe na direction moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais anafanya kazi nzuri sana nimemwona akizunguka, anahamasisha biashara na anasema mfanyabiashara akiwa na shida aniambie mimi moja kwa moja. Hivi kweli wote tutamfikia Mheshimiwa Rais kumwambia matatizo yetu wakati Mawaziri wapo? Wamsaidie Mheshimiwa Rais kufanya kazi hizi, wamsaidie kabisa. Haiwezekani Mheshimiwa Rais kila wakati anazunguka anapiga kelele mpaka anasema watendaji mnaonekana hamnielewi, kama hawamwelewi basi waachie ngazi, ndiyo, it’s true. Tunataka sisi Tanzania ambayo inasonga mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kusema kwamba leo hii kuna miradi ya kimkakati, Mchuchuma na Liganga kila siku ni hadithi na ngonjera. Mheshimiwa Waziri atapokuwa ana-wind up hapa naomba nipate taarifa sahihi kwamba suala la Mchuchuma na Liganga tunatokaje hapa tulipo? Kila siku sisi tunasema, tunajadili, mwaka huu tunajadili, mwaka unaofuata tunajadili; tunafika wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme kingine, Mheshimiwa Dkt. Kingwangala yuko hapa hivi, watu wanapoingia hapa nchini it’s part of the business. The first impression anayoipata hapa anapoingia pale airport, anakuta wafanyakazi wa airport wamenuna kama wamekula pilipili. Wewe unamkaribisha mgeni nyumbani kwako umenuna, unaweza kum-harass mtu, why? Katika nchi nyingine unapokwenda unapewa a very good treatment, lakini hapa akija mgeni ni kama amekuja kwenye madaladala. (Makofi)

T A A R I F A

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba unilindie muda wangu nadhani Mheshimiwa Waziri hakunielewa.

WABUNGE FULANI: Kweli kabisa.

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuelewa concept yangu mimi, siyo suala la kutabasamu na kuvaa uniform nzuri ni culture ya kupokea wageni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wewe kama Waziri mwenye zamana hii hiyo unapaswa uonyeshe kwamba, unajua sikiliza unapompokea mgeni, its all inclusive package, hata tabasamu ni sahihi, hata ku-facilitate kupata mizigo au permit vyote ni muhimu zaidi na kadhalika, wewe kama Waziri wa Utalii unapaswa kuibeba hiyo.