Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi ili nami niweze kuchangia katika Wizara hii ya Wiwanda na Biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia afya mzuri na leo hii nikaweza kusimama katika Bunge hili. Pia nitoe pongezi zangu za dhati kabisa kwa Fulbright Prof. Ibrahimu Haruna Lipumba kwa kuchaguliwa na Wajumbe wa Mkutano Mkuu Taifa kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF. Nitoe pongezi zangu za dhati kabisa kwa Mheshimiwa Muftaha Abdalla Nachuma kwa kuchaguliwa na Wajumbe wa Mkutano Mkuu Taifa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF. Vilevile nitoe pongezi za dhati kabisa kwa Baraza Kuu la Uongozi wa Taifa kwa kumchagua Mheshimiwa Magdalena Hamis Sakaya kuwa Naibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, azma ya Serikali ni kuelekea Tanzania ya viwanda. Katika kuelekea Tanzania ya viwanda hatua ya kwanza ni kuondoa urasimu pale wanapokuja wawekezaji kwa kuwapatia maeneo ya ujenzi haraka na mapema iwezekanavyo. Hata hivyo, Wizara ya Viwanda kumekuwa na urasimu na kodi kubwa hali inayopelekea baadhi ya wawekezaji kuhamia nchi jirani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano ni Kiwanda cha Kubangulia Korosho cha Olam ambacho kilikuwa katika Mkoa wa Mtwara. Kiwanda kile kilifanya kazi vizuri sana na kuliweza kutoa ajira kwa wanachi wa Mkoa ule vijana na akina mama waliweza kuendesha maisha yao kupitia kiwanda hicho lakini mpaka sasa napozungumza kiwanda hicho hakipo kimehamia nchini Msumbiji. Je, Serikali haioni kuwa inakosa mapato na ajira kwa Watanzania? Nataka commitment ya Serikali hali hii ya kuhamahama wawekezaji katika nchi yetu itaisha lini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapoimarisha viwanda nchini tunahitaji malighafi (materials) zinazozalishwa na wakulima wetu. Wakulima wakiwa na masoko ya uhakika wataweza kuongeza juhudi za uzalishaji wa mazao ambayo ndiyo malighafi viwandani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee Shirika la Viwanda Vidogovidogo (SIDO). Tanzania tunalo Shirika la Viwanda Vidogovidogo (SIDO) lakini hatulitumii ipasavyo kwa sababu SIDO wanabuni na kutengeza mashine na mitambo mbalimbali inayoweza kutumika katika kilimo, ujenzi, nishati, uchimbaji wa visima, lakini havitangazwi. Tumekuwa tukiona karakana nyingi za SIDO mitambo yake ni chakavu na haifanyi kazi kabisa matokeo yake wananchi na Serikali wanatumia fedha nyingi kununua mashine na mitambo mbalimbali kutoka China. Natoa wito kwa Serikali itumie teknolojia yetu mzuri ya SIDO. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee suala la wafanyabiashara wadogo wadogo. Ni ukweli kuwa akina mama wengi ndiyo wafanyabiashara ndogondogo na za kati, lakini nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kuliona suala la vitambulisho kwa wajasiliamali wadogo wadogo. Pia niishauri Serikali akina mama lishe, wauza matunda, maandazi, samaki, wasamehewe au walipe kidogo kidogo kutokana na kipato chao kuwa kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)