Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa fursa kuchangia Wizara hii, jambo moja la kwanza kabisa kabla sijaanza kutoa mchango wangu, nataka niiombe Serikali, Wizara ya Fedha, waangalie huu Mwezi wa Ramadhan, kuna request kubwa za Taasisi mbalimbali za Kiislam ambazo zimeleta tende na vyakula kwa ajili ya kutoa sadaka kwa watu maskini ziweze kupata request ya exemption ambazo wameomba kutoka Tanzania Revenue Authority. Taasisi hizi ziko regulated chini ya BAKWATA na zimepeleka requests zake na wengi wanatoa katika maeneo ambayo watu wana umaskini mkubwa, they cannot afford kupata futari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu utajikita katika maeneo makubwa yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ni suala la kufanya biashara; biashara yoyote duniani, ina mambo makubwa mawili na ninachomshukuru Mwenyezi Mungu, Rais Magufuli alivyoingia madarakani, aliweka vision yake clear, kwamba anataka kujenga nchi yenye uwezo wa kujitegemea ya viwanda. Hii ndiyo vision, ni matarajio yangu mimi na wengine wote tuliomo humu na Watanzania, kwamba wanaomsaidia Mheshimiwa Rais kusaidia utekelezaji wa vision hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, biashara ina mambo mawili, moja kuna software part of business na upande mwingine ni hardware part of business. Hardware part of business, tunajenga barabara, tunajenga reli, tunanunua ndege, tunajenga miundombinu ya umeme, lakini hii hardware part ya biashara, isipokuwa compatible ya software part ya biashara ambayo ni regulation na sheria, hii itakuwa ni wastage ya resources. Kama tutajenga reli, tutajenga barabara, tutaleta umeme, vyote hivi vikakosa biashara ambayo itavifanya hivi vitu viwe effective, havitakuwa na maana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nataka nitoe mifano michache, kwenye Kamati yetu ya Bajeti, walikuja watu wa CTI. CTI kwenye presentation yao, ambayo ninayo hapa na bahati nzuri Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara tulikuwa naye, wanazungumzia existence of multiple Regulatory Authority leading to high costs of doing business, kwa sababu biashara vilevile gharama ni jambo la msingi. Sasa anakwambia an example for the food processing industry is registered by more than 15 authorities, taasisi 15 zina-regulate food processing industry.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pharmaceutical industry, ili aanzishe biashara ya kiwanda kidogo cha pharmaceutical industry na huyu mtu aliyekuja kufanya hii presentation ni mtu ambaye anataka kuweka kiwanda Mkoa wa Mwanza kwa ajili ya kutumia pamba iliyoko pale kutengeneza pamba kwa ajili ya mahospitali. Huyu mtu, anahitaji regulatory authorities zimepe jumla la ya leseni 26 ili aweze kuanzisha huu mradi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, a registered company kwa ajili ya ku-export horticulture products, maua na bidhaa zingine za hotculture, anahitaji kupata jumla ya vibali 45 ili aweze ku-export biashara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiwanda kwa ajili ya kuzalisha maziwa ana tozo na kodi na leseni jumla 26 ili anzishe kiwanda hicho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwape mfano, kuna kiwanda kidogo kiko Nanenane hapa Dodoma, mwaka 2016 aliamua kuanzisha kiwanda chake cha ku-process asali ambacho kina uwezo wa ku- process tani 3 kwa siku. Februari 2016 na ninazo barua zake hapa, huyu mwananchi ameiandikia TFDA ije ikague kiwanda chake iangalie mfumo wa uzalishaji na kumpa approval amejibiwa Novemba 6, barua ya kwamba tutakuja kukagua. Mpaka amepata certificate ni Februari 2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu ni mfanyabiashara mdogo, kachukua mkopo Tanzania Investment Bank wa shilingi milioni 200, benki sasa iko mlangoni kwake inataka kuli-recall mkopo wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nini sasa ushauri wangu? Ushauri wangu ni hivi, ile taarifa ya IMF iliyo-leak (unofficial), imetupa mambo mazuri mno na mimi nataka nishauri Serikali ipokeeni kwa sababu imetupa two options, imetuambia kama tunataka ku-grow kwenda 6%, 7% kuna mambo manne ya kufanya. La kwanza improve business environment.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu TFDA, OSHA, taasisi zote hizi anzisheni one building wawekeni pale andikeni business facilitation of whatever ili mfanyabiashara akishachukua leseni yake ya usajili wa Kampuni BRELA, the second place anayoenda anaenda kwenye business facilitation building. Akifika pale analipia taasisi zote na muweke chini pale cage kama za benki, iwe imeandikwa NEMC, TFDA, TBS, ndani ya jengo moja. Yule mfanyabiashara aki-launch application yake pale and the world is connected, akitoka anatoka na document zake anaenda kufanya biashara yake, hili ni jambo muhimu mno. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingne ambalo nataka niulize, TBS ana evaluate standard ya bidhaa na vitu ambavyo tunazalisha. Kama mtu kapata certificate ya TBS anazalisha maziwa kwa nini tena akatafute certificate ya TFDA? Wawekeni hawa watu wote ndani ya one umbrella TFDA awe unit ndani ya TBS ili mtu akiingia afanye kila kitu mule, OSHA awe unit ndani ya NEMC may be ili tuangalie namna gani ya ku-harmonize mambo haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe kaka yangu Waziri Kakunda, blueprint leta sheria. Kama kuna mahitaji ya mabadiliko ya sheria jamani mwaka wa fedha huu upo bado hatujamaliza, hata kama ni weekend moja tukae hapa tuwasaidieni kufanya haya mambo yawe rahisi katika kufanya biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nitoe mfano, hapa mkononi nina taarifa leather sector. Sijui kama Kanuni zinaruhusu ni vizuri sana kwenye Kamati ya Bajeti Waziri Jenista awe anakuja, hili ni ombi ili aone mambo yalivyo ndani ya Serikali. Yeye yuko pale kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu kwa ajili ya ku-coordinate Mawaziri na taasisi za Serikali inakuwa rahisi center of coordination ya shughuli za Serikali kutokea Ofisi ya Waziri Mkuu kuwepo, ni muhimu na nasema hii from my heart kwa sababu kuna mambo yanafanyika unajiuliza are we one Government? Inasikitisha! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikupe mfano, usafirishaji wa ngozi wet blue, mwaka 2016 tulisafirisha ngozi wet blue pieces 1.2 million kwenda nje, leo tuna export wet blue pieces 200,000. Wet blue ni stage ya kwanza ya ku- process, ngozi kutoka raw kwenda wet blue ni stage ya kwanza ambapo tumesafirisha 1.2 pieces mwaka 2016 leo tume export only 200,000 pieces, hii hapa taarifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, unajiuliza swali kama tunazalisha pieces milioni 3 kwa mwaka kama nchi hizi zinazobaki ambaz hatujasafirisha ziko wapi? Ukienda kuangalia raw exported only iliyokuwa exported ni pieces 400,000 kuna pieces zaidi ya 800,000 vimeondoka under smuggling na mnajua ni kwa nini? Ni kwa sababu ya one thing, tume impose 10% export levy ya wet blue ambayo competitors wetu wote kwenye East Afrika hawana kodi hiyo, tunayo sisi. Ni kwa sababu gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulienda Arusha tukasaini makubaliano ya Afrika Mashariki tukaingizwa mkenge halafu wao wenzetu hawatekelezi sheria hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, hapa tumesikia suala la Mchuchuma na Liganga, Waheshimiwa Wabunge hebu tujiulize swali, kwenye Mradi wa Mchuchuma na Liganga kuna Mradi wa Makaa ya Mawe, Mradi wa Chuma, Mradi wa Umeme na mradi wa kuchakata product zinazotokana na chuma, sasa wapi tumekwama? Ukisikiliza kabisa kutoka NDC mkwamo unatokana na umeme na chuma. Sasa nauliza kama miradi miwili ina matatizo, kwa nini tunazuia utekelezaji wa mradi wa makaa mawe? Kwa nini hii miradi yote minne tunaifunga pamoja ukifa mmoja they entire project is dead. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama tunaona kuna matatizo tunapeleka barabara Liganga na Mchuchuma, tunapeleka line kubwa ya umeme, why are we spending that money kupeleka kule kama nchi? Kwa nini tusipeleke kwenye madarasa au kwenye maeneo mengine? (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Bashe, nilikuongezea dakika tatu.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, ahsante. (Makofi)