Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Spika, napenda kutoa pongezi za dhati kwa Wizara hii kwa ujumla wao kwa maslahi ya wananchi wetu, ni wizara pana ndani ya utekelezaji wake, hivyo nasisitiza na kukubaliana na Kamati na kupongeza kwa kuongezewa bajeti, lakini ni bora zaidi ikiwa Hazina watazitoa zote au kwa asilimia zaidi ya 85.

Mheshimiwa Spika, kwani tunatarajia kuinua utalii ambao unatupatia mgawo wa zaidi ya asilimia tano ya pato la Taifa, pia kurahisisha mawasiliano ya barabara kwa uchumi wa nchi yetu. Tunashukuru jitihada ya Serikali ya kutuunganisha na nchi jirani kwa barabara ya kiwango cha lami, Sumbawanga – Matai – Kassanga (DRC CONGO), Matai – Kasesya (Zambia). Ombi, tunaomba kasi kuongezwa kwa ukamilifu wa barabara hizi pamoja na kuwemo kwenye bajeti iliyobainishwa ukurasa wa 257, tunasisitiza fedha za miradi ya maendeleo kutolewa zote na kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, hali ya barabara ya bonde la Rukwa kutoka Kibaoni hadi Kilyamatunda ina hali ngumu kutokana na maji yanayoporomoka kutoka mlimani na kuelekea Ziwa Rukwa, yanakuwa na nguvu na kukokota miti mikubwa na kuhatarisha madaraja katika barabara hiyo yote na yote yameharibika na kupelekea kila mwaka kurekebishwa maeneo korofi na kuendelea kutumia pesa nyingi za walipa kodi.

Mheshimiwa Spika, mapendekezo na ushauri, barabara hii ni kutengenezwa kwa kiwango cha lami na ujenzi wa madaraja makubwa na madhubuti, ndiyo suluhisho lake. Pamoja na Bajeti iliyopendekezwa kwa baadhi ya maeneo katika ukurasa 302, Ntendo – Muze, Ilamba – Kaoze, Kasansa – Kilyamatundu, Mtowisa – Ilemba, ni matumaini yangu, ushauri wa muda mrefu wa ujenzi wa barabara hii kuliko ilivyo sasa.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Rukwa, tuna Kiwanja cha Ndege, Sumbawanga ambacho kinafanyiwa ukarabati na kuongezwa urefu wa uwanja huo, kwa kiwango cha lami, ili nasi tupate usafiri wa Anga. Ombi, tunaomba kasi kuongezwa katika kuendeleza ukarabati huo, ambao haujaonekana ipasavyo, kwani tuna kiu kubwa na kukamilishwa mradi huo kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, bado nasisitiza Wizara kuangalia uwezekano wa kuweka utaratibu wa kuzijenga barabara za mabonde ya Rukwa na Tanganyika kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, mwisho, naunga mkono hoja.