Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Muhammed Amour Muhammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Bumbwini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED: Mheshimiwa Spika, awali ya yote naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu wa rehema kwa kunipa uhai na uzima na pia kuniwezesha kuchangia mada iliyopo hewani kwa lengo la kulipaisha Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, nianze na Bandari ya Bagamoyo. Ni vyema Serikali ingefikiria zaidi kujenga Bandari ya Bagamoyo. Hii itasaidia kuimarisha uchumi wa maeneo hayo na pia kuongeza Pato la Taifa. Bandari ya Bagamoyo kama itajengwa, hata hii Reli ya Kati nayo ndiyo itaweza kufanya kazi vizuri, mizigo itapatikana kutoka nchi tofauti kuletwa hapa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, usajili wa simu; kwa masikitiko makubwa sana, TCRA haionekani kutoa mashirikiano mazuri na Zanzibar (SMZ). Kwa upande wa Zanzibar ZAN – ID ndiyo kila kitu, ndimo yalimo maisha ya Wazanzibari. Ni vyema basi kama ZAN – ID nayo ikatumika katika usajili wa simu.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa bandari ni masuala ya Muungano, kule Zanzibar bandari zake zimekuwa hovyo sana na zimeachwa kama hazina mwenyewe, je, Serikali ya Muungano ina mpango gani kuhusiana na maboresho ya bandari za Zanzibar?

Mheshimiwa Spika, wizi wa mitandaoni; kumekuwa na wizi mkubwa wa wananchi katika miamala ya fedha. Kwa mfano kama utamtumia fedha mdogo wako na kwa bahati mbaya usipate wakati wa kumuarifu, baada ya muda basi anapigiwa simu na mtu mwingine kama yeye ndiye aliyemtumia fedha na azirejeshe na namba ya kurejesha anatoa na hii inarudi kwa mwizi. Zikitakiwa namba zilizotumika ninazo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.