Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Spika, nipende kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Jangwani; nipende kujua nini sababu ya ujaaji wa maji, baada ya matengenezo ya mwendokasi ndiyo imekuwa mbaya kuliko. Swali; je, upembuzi yakinifu haukufanyika au ilikuwaje, kila ikinyesha mvua lazima watu washindwe kupita barabara hii? Leo hii tunavyoongea Jangwani hakupitiki; je, hivi kweli wananchi wanazunguka na kupoteza muda mwingi kutafuta jinsi ya kufika kazini kwao?

Mheshimiwa Spika, barabara na fidia kwa wananchi wa Kibaha wanaopisha upanuzi wa barabara TAMCO – Mapinga. Wananchi wanashindwa kujua hatma ya maisha yao kufuatia tathmini iliyofanywa na malipo kukwama, hivyo kusababisha wananchi kuwa na umaskini uliokithiri. Serikali irudi kwa wananchi iwaambie wamekwama wapi kulipa fidia iliyowaahidi miaka minne iliyopita.

Mheshimiwa Spika, magari ya mwendokasi; najua kuwa SUMATRA ambao wanatetea pia wasafiri ambao ni idara katika Wizara hii. Usafiri wa mwendokasi ni shida sana, magari ni machache sana na wasafiri ni wengi, hivyo kupelekea wasafiri kujazana sana mpaka kukosa hewa na kusababisha wengine ku-faint kwa kukosa hewa. Nini maana ya kugharamia mradi huu na kuondoa mabasi ya kawaida, wananchi hawaielewi nia ya Serikali kuondoa magari ya kawaida, Serikali imewapa mateso makubwa kwa kuleta mradi huu.

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa majengo kwa ajili ya kuuza. Ujenzi unaojengwa na TBA usiangalie upana wa viwanja na ubora wa majengo wanayoyajenga ambayo inapelekea wananchi kushindwa kununua kutokana na udhaifu unaopelekea wanunuzi kuona nyumba hizi sio rafiki kwa maisha yao.

Mheshimiwa Spika, TEMESA; matengenezo yanayotokana na TEMESA ukipeleka gari kutengenezwa inatengenezwa kwa muda mrefu kuliko yanayotengenezwa kwa watu binafsi. Hata barabarani taa zote zinapoharibika urekebishaji ni shida.

Mheshimiwa Spika, bandari; nishauri Serikali kujifunza utoaji huduma wa Bandari za Durban, Beira na Mombasa, vinginevyo wateja watatukimbia iwapo urasimu wetu na tozo nyingi utaendelea katika Bandari ya Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika, TTCL; tumeimba mara nyingi sana kuwa Serikali ilipe madeni inayodaiwa pia itoe uhuru wa uendeshaji ili ijiendeshe kibiashara, iwe na uwezo wa kukopa na kukopesha.