Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Spika, naomba kumpongeza sana Mheshimiwa Engineer Kamwelwe, Waziri na Naibu Mawaziri kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kutekeleza majukumu yao. Serikali kupitia ahadi ya Mheshimiwa Rais, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli aliahidi kutengenezwa kwa Barabara ya Nyashumo – Ngasamo – Dutwa, kilomita 45 kwa kiwango cha lami. Huu ni mwaka wa nne, ningependa kujua ni lini ujenzi wa kiwango cha lami utaanza ili kuwezesha usafirishaji wa bidhaa za kilimo pamoja na usafiri wa wananchi uweze kutekelezwa? Aidha, kumekuwepo na uimarishaji wa madaraja na baadhi ya sehemu korofi kwa kiwango si cha kuridhisha. Hivyo naomba kupata majibu ni lini sasa ujenzi huu wa barabara utaanza.

Mheshimiwa Spika, ahsante.