Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Spika, pamoja na mchango wangu niliochangia katika Bunge lako Tukufu leo; nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kumteua Waziri wa Ujenzi Engineer Kamwelwe ambaye natambua uchapa kazi wake, akiwa Naibu Waziri wa Mji alifanya kazi kubwa sana na kuwasaidia sana wananchi wa Jimbo langu. Pamoja na kazi kubwa aliyoifanya, pamoja na mchango wangu wa kuongea Bungeni, nimwombe Waziri azingatie yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, nampongeza Waziri kwa kukubali ujenzi wa barabara ya Nyamwage – Utete kilomita 33, barabara hii ni ahadi ya Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ya tarehe 4/3/2017 kuwa itakamilika kabla ya 2020. Nimwombe Mheshimiwa Waziri sasa kwa kuwa upembuzi yakinifu umekamilika, aje sasa kuweka jiwe la msingi mwezi Juni ili wananchi wapate imani kwani barabara hii imeondoa Wabunge wengi.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali inisaidie ili niweze kurudi 2020 – 2025. Nyamwage-Utete ni kiini cha anguko la kiuchumi Rufiji, ubovu wa miundombinu ni kero kubwa kwa wananchi, Mheshimiwa Waziri afike sasa Rufiji ili kuanza ujenzi wa barabara hii, pamoja na barabara ya Nyamwage Utete. Niombe Serikali ikubali ujenzi wa barabara ya Kibiti - Mloka ambayo inasaidia wakandarasi wanaojenga mradi wa umeme wa Rufiji (Stiegler’s). Barabara hii ni chafu sana na haifai. Mradi huu wa umeme utachelewa sana iwapo barabara hii haitajengwa kwa kiwango cha lami. Ipo barabara ya Ikwiriri – Mloka ambayo ni kioo cha uchumi wa Rufiji, tunaomba Serikali kuiweka katika mpango wa ujenzi wa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, ipo barabara ya Utete – Ngarambe, hii ni muhimu sana kufungua utalii wa Pwani ya Kusini. Ngarambe kuna Selou na pia kuna vipepeo vinavyoweza kuvutia watalii.

Mheshimiwa Spika, nyingine ni barabara ya Mloka - Kisarawe, Mloka - Kisaki, Bungu – Nyamisati – Kisiju - Mkuranga, Vikindu – Vianzi. Hizi ni barabara muhimu kwa kufungua uchumi wa Mkoa wa Pwani, ubovu wa miundombinu hii kumepelekea kudumaa kwa uchumi na ndiyo sababu kumekuwepo na wimbi kubwa la umaskini katika eneo la Pwani ya Kusini.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.