Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE: Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri Kamwelwe, kwa kazi nzuri sana anayoifanya kuiongoza Wizara hii. Niwapongeze sana Manaibu Waziri Mheshimiwa John Kwandikwa na Mheshimiwa Engineer Atashasta Nditiye na Makatibu Wakuu wote kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Rais wetu kwa kutujengea barabara ya Mwanga – Kikweni – Vuchama – Ngofi – Kiriche - Lomwe kwa kiwango cha lami. Sisi Wanamwanga tunamshukuru sana. Pia tunawashukuru sana kwa kuzipandisha barabara za Lembeni – Kilomeni - Ndorwe na barabara ya Kirya - Lang’ata Bora - Kifaru kuwa barabara za TANROADS.

Mheshimiwa Spika, suala langu la tatu ni mawasiliano, tunaishukuru sana Serikali kwa kulea uwekezaji katika mawasiliano. Hakika karibu nusu ya Watanzania wanamiliki simu ya mkononi, aidha, bei za kutumia mitandao ya simu zimeendelea kushuka. Hata hivyo, makampuni ya simu yanatumia ujanja na control ya system nzima kuwaonea na hata kuwaibia wananchi wanaotumia mitandao yao. Unanunua kifurushi cha GB 15 kwa Sh.20,000/=, kwa siku saba, unatumia GB 3 kwa siku zote saba, halafu GB 12 zinamezwa kwa kuwa siku saba zimekwisha. Huu ni wizi, mtumiaji wa simu akinunua kifurushi ni chake, lazima atumie mpaka kiishie ndiyo anunue kipya. Huu ndiyo utaratibu wa kununua na kuuza mali.

Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa fursa.