Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Spika, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Serikali ya CCM kwa kutumia zaidi ya bilioni mia mbili kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Daraja la Mto Sibiti ambalo litaunganisha Mkoa wa Simiyu na Singida na kunufaisha kiuchumi na kijamii wananchi wa Mkoa wa Simiyu hususan Wilaya ya Meatu. Naomba kusaidiwa yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza, kujenga kwa kiwango cha lami kilomita 25, ahadi iliyotolewa na Mheshimiwa Rais wakati wa uzinduzi wa daraja. Pili, Daraja la Mto Sibiti halitakuwa na tija wakati mvua kubwa itakaponyesha mfululizo kama makorongo ya Itembe na Chombe yaliyopo barabara ya kutoka Sibiti hadi Mji wa Mwanhunzi hayatajengewa madaraja ya juu. Naomba makorongo hayo yajengewe daraja ili kuwepo na thamani ya pesa kwa daraja hilo kupitika kwa uhakika na magari ya aina zote.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.