Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru wewe binafsi kwa kunipa nafasi katika kuchangia mchango wangu na ushauri kwa Serikali katika Wizara hii ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM Serikali iliahidi kutekeleza ujenzi kwa kiwango cha lami katika barabara ya Singida – Sepuka – Ndago – Kizaga yenye urefu wa takriban kilometa 92. Barabara hii imekuwa barabara muhimu sana kwa sababu ya uzalishaji mkubwa wa mazao ya biashara kama vile alizeti, mahindi na kadhalika. Wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2015 Mheshimiwa Rais alipita barabara hii na kuwaahidi wananchi kuwa barabara hii itajengwa kama ambavyo Ilani ya Uchaguzi wa CCM ilielekeza, lakini mpaka hapa tunapoongea utekelezaji wa Ilani katika ujenzi wa barabara hii bado unasuasua na hivyo kuwafanya wananchi kuendelea kupata adha katika kusafirisha mazao na hata mafuta yanayozalishwa katika viwanda ambavyo vimejengwa maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, Serikali yetu imekuwa ikitumia sana fedha nyingi katika matengenezo ya muda mfupi na mrefu ya barabara hii, jambo ambalo kama Serikali itaweka dhamira ya dhati katika kujenga barabara hii kwa Mwaka wa fedha 2018/19 Serikali ilitenga fedha za upembuzi yakinifu wa barabara hii lakini mpaka leo hatua za utekelzahi haueleweki.

Mheshimiwa Spika, katika Sekta hii hii ya barabara, Serikali tangu mwaka 2010 imejenga madaraja katika barabara ya Sepuka – Mkandala – Mgungira tangu madaraja yakamilike leo miaka 9 ujenzi wa tuta la barabara umeshindikana, hivi tumetumiaje pesa za umma kwa mamilioni na kushindwa kukamilisha ujenzi wa tuta tu? Barabara hii ni muhimu sana katika kusafirisha mazao ya chakula na biashara kama vile mchele, alizeti na barabara hii ambayo inaungana na barabara ya Magereza –Mtuduru – Iyumbu imekuwa ya muda mrefu sana mvua zimenyesha watu hawa wanakosa mawasiliano. Ni muda muafaka sasa kwa Serikali kutekeleza ujenzi wa barabara hii muhimu kwa wapiga kura wa Jimbo la Singida Magharibi.

Mheshimiwa Spika, jambo la tatu, mawasiliano ya minara ya simu; jiografia ya Jimbo la Singida Magharibi iko very complicated. Toka nimekuja Bungeni tumekuwa tukipewa vitabu vinavyoonesha distribution ya minara ya simu, lakini hakuna utekelezaji wa mnara hata mmoja ambao uliahidiwa na Serikali ambao umejengwa.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2018 wananchi wa Kata ya Iyumbu walivamiwa na majambazi mchana na maduka yote kuporwa pesa, watu wetu hawakuweza kupata msaada sababu ya ubovu wa barabara na ukosefu wa minara ya simu, hakuna mawasiliano ya barabara wala ya simu na kata hizo ndizo zinaendesha halmashauri ya Wilaya ya Ikungi ambapo asilimia 90 ya mapato yanatoka kule kutokana na kiwango kikubwa cha uzalishaji wa mchele ambao unauzwa Uganda, Rwanda na Burundi na kuliletea Taifa mapato ya ndani.

Mheshimiwa Spika, mwaka jana vilitolewa vitabu hapa ambavyo TTCL wamepewa market share ili kufungwa minara katika maeneo hayo, lakini hakuna lolote lililofanyika katika kuwasaidia Watanzania hawa.

Mheshimiwa Spika, haya mambo yanatuweka mahali pagumu sana. Naomba minara ya mawasiliano ikafungwe Ikungi, Igholwe na maeneo yote ambayo wananchi wanapata matatizo katika Jimbo la Singida Magharibi.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.