Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Mheshimiwa Spika, miradi mbalimbali ya ujenzi wa viwanja vya ndege inaendelea katika Mikoa mbalimbali kama vile Msalato, Tabora, Kigoma, Mpanda, Mtwara, Shinyanga, Kilimanjaro, Sumbawanga, Arusha, Songwe na Mwanza. Kazi kubwa zinazofanyika katika miradi hiyo zinajumuisha ujenzi wa barabara za ndege, upanuzi na ukarabati wa maegesho ya ndege, ujenzi wa vituo vya waangalizi wa hali ya hewa, ujenzi wa barabara za kuingilia viwanja vya ndege, uboreshaji wa viwanja hivyo pamoja na ujenzi wa majengo ya abiria na mizigo.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kazi zote hizo zinazoendelea bado kuna matatizo makubwa ya viwanja vingi kukosa uzio, tumeshuhudia Kiwanja cha Ndege cha Mwanza mtu aliyekatisha ndani ya kiwanja wakati ndege inaruka na kusababisha ajali. Lazima Serikali ihakikishe kila kiwanja cha ndege kinachojengwa na uzio unajengwa kuepusha madhara yanayoweza kutokea kwa wanyama na binadamu wanakatisha ndani ya kiwanja hata Kamati ilipotembelea Kiwanja cha Dodoma mbwa alikatisha.

Mheshimiwa Spika, Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote UCSAF ulianzishwa na Serikali kwa Sheria Na. 11 ya mwaka 2006 ukiwa na lengo la kupeleka huduma ya mawasiliano maeneo yasiyokuwa na mvuto wa kibiashara. Mfuko huo umejitahidi kupeleka huduma hiyo lakini bado maeneo mengine yasiyo na mvuto wa kibiashara hayajapata huduma hiyo. Tunaiomba Serikali ifanye kama kusudio la sheria iliyoanzisha Mfuko huo lilivyo ili Watanzania wote huduma hiyo kwa ajili ya kuleta maendeleo.