Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, kivuko kipya kati ya Bugorola – Ukara. Pamoja na jitihada za Serikali kuanza mchakato wa utengenezaji wa kivuko kipya baada ya ajali ya MV Nyerere, mchakato huu unaenda taratibu. Kivuko kilichopo sasa cha MV Saba Saba kina matatizo mengi hali inayoendeleza hofu kwa watumiaji wa kivuko hiki. Ombi, kivuko hiki kikikamilika mapema ili kinusuru maisha ya watu wetu. Pia uangaliwe uwezekano wa kuweka usafiri wa uhakika kwenye maeneo ya Kitale – Irugwa na Kakukuru – Gana.

Mheshimiwa Spika, upatikanaji wa kifusi kwa ajili ya utengenezaji wa barabara. TANROADS wamekuwa na kawaida ya kuchimba kifusi/changarawe pembezoni mwa barabara jambo ambalo limekuwa linaacha mashimo makubwa sana na kusababisha vifo. Mfano, wiki iliyopita tarehe 9 Mei, 2019 shimo lililochimbwa kwa ajili ya kifusi eneo la Kijiji cha Nakamwa, Kata ya Namilembe, Wilaya ya Ukerewe limesababisha vifo vya watu wawili baada ya gari kutumbukia katika shimo hilo. Hii ni moja ya matukio ya kifo na majeruhi ambayo yamekuwa yanatokea mara kwa mara Wilayani Ukerewe. Ushauri, baada ya shughuli za ujenzi wa barabara mashimo haya yamekuwa yanafukiwa.

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa barabara ya lami; kwa kuwa barabara ya Bukindo – Murutunguru – Bukonyo ni muhimu sana kwa uchumi wa ukerewe na sehemu ya barabara hii ilishafanyiwa upembuzi yakinifu, michoro na makadirio tayari yalishaandaliwa tayari yakisubiri upatikanaji wa fedha ili ijengwe. Naomba Wizara isaidie upatikanaji wa fedha ili barabara hii iweze kujengwa kwani ni kilometa saba tu.

Mheshimiwa Spika, wakati wa ujio wa Mheshimiwa Rais Visiwani Ukerewe tarehe 5 Septemba, 2018 aliahidi ujenzi wa barabara kilometa 14 kutoka Lugezi – Nansio kwa kiwango cha lami. Naomba Serikali itekeleze ahadi hii.