Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa fursa ya kuchangia hoja hii muhimu sana kwa maendeleo ya nchi yetu. Namshukuru Mungu kwa rehema na neema yake kwa Bunge letu na uongozi mzima. Pia nampongeza Mheshimiwa Waziri Kamwelwe na Manaibu wake wote na watendaji kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, Wilaya yangu ya Ileje imepata fedha za kujenga barabara kuu ya Mpemba - Isonpole kwa kiwango cha lami na tayari kazi imeanza. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa barabara hii ambayo ilikuwa ni ahadi yake na vile vile iko kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2015. Ahsante sana Mheshimiwa Rais, wana Ileje wana deni kubwa kwake, wameingoja barabara hii miaka 42.

Mheshimiwa Spika, ziko barabara za TARURA Wilayani Ileje ambazo kwa ugumu wake hazitaweza kujengwa na TARURA. Tulipeleka maombi ili zifikiriwe kujengwa na Wizara ya Ujenzi. Aidha, kuna barabara ambazo madaraja yalikatwa na mvua tangu 2016 na kwa hivyo wananchi wa Chitete na Mlale hawana mawasiliano kupitia Ilanga kitongoji kinachopakana na Wilaya ya Vwawa. Tunaomba sana watufikirie wana Ileje watupatie fedha za kujenga miundombinu ya Ileje, kwani ni migumu sana na hii imekuwa kikwazo kikubwa cha maendeleo ya kiuchumi kwa Wilaya ya Ileje.

Mheshimiwa Spika, naambatanisha kwa barua husika maombi yetu kwa maandishi ili watufikirie.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.