Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia Wizara hii ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ambayo ni Wizara muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa letu kwenye maeneo tofauti ili kuinua uchumi kama ifutavyo:-

Mheshimiwa Spika, TARURA waongezewe fedha. Suala hili limekuwa na changamoto kubwa sana, kwani TARURA wana barabara nyingi za mitaa na vijiji lakini wanashindwa kumaliza kazi hizi kwa muda muafaka kwa sababu ya fedha kidogo.

Mheshimiwa Spika, lingine ni usafiri wa meli kwa Ziwa Tanganyika. Kumekuwa na changamoto kubwa ya usafiri wa majini kwa wananchi wanaotumia Ziwa Tanganyika kwa usafiri na biashara. Naomba kujua Serikali imefikia wapi katika suala la Meli ya MV Liemba?

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na malalamiko ya Wakandarasi wengi kutokulipwa fedha zao kwa wakati. Kwa nini Serikali isiwalipe Wakandarasi ili kuleta ufanisi kwa kazi na miradi wanayopewa ili kuinua uchumi wa nchi?

Mheshimiwa Spika, ni vyema kufuatilia na kujua uwezo halisi wa Wakandarasi kabla ya kupewa tenda ili kuepusha hasara zinazoweza kujitokeza kwa Taifa, kwani kumekuwa na malalamiko mengi sana na kupelekea vitendo vya rushwa na kupelekea hasara kwa Taifa.

Mheshimiwa Spika, suala la ujenzi wa viwanja vya ndege ni vyema liangaliwe kwa umakini kwa kuangalia aina ya watu kwa maeneo ambayo wana uhitaji wa viwanja vya ndege ili kuweza kukuza uchumi kwa eneo husika na Taifa kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, suala la TBA bado kuna changamoto; miradi mingi wanayopewa haikamiliki kwa wakati. Pia napenda kuishauri Serikali ipunguze miradi kwa TBA na badala yake wapewe watu wengine ambapo kukiwa na ushindani huleta ufanisi mzuri wa kazi na uharaka.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la watu kuwekewa X za kijani na nyekundu: kumekuwa na mkanganyiko katika utekelezaji wa suala hili pale inapotokea nyumba moja ina alama mbili ya kulipwa na kubomolewa, wanawaambia wananchi wabomoe. Je, suala hili likoje? Tunaomba ufafanuzi.