Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa mchango ufuatao:-

Mheshimiwa Spika, naomba barabara ya Kitosi – Mwampembe yenye urefu wa kilometa 67 ambayo ni mkombozi kwa Tarafa ya Wampembe ichukuliwe na Serikali au la, iwe inapewa fedha ya kutosha toka TANROADS. Wizara inatoa shilingi 90,000/=, inatosha nini? Tafadhali naomba tuwe tunaipa fedha zaidi.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Nkara – Kala ni ya Halmashauri/TARURA lakini haipewi fedha. Adha zinazowapata wananchi wa Kata ya Kala inatakiwa iondolewe na Serikali. Tafadhali ongezeni fedha TARURA ili iwe na uwezo wa kusaidia wananchi vijijini.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Katongoro kwenda Ninde haipitiki kabisa, kisa hakuna fedha ya kuhudumia barabara hiyo ya kwenda Ninde na kata yote isifikiwe. Tafuteni fedha kuimarisha TARURA.

Mheshimiwa Spika, lingine ni kuhusu mitandao ya simu. Naomba vijiji vifuatavyo vipate mawasiliano ya simu: Kijiji cha Kasapa, Kata ya Sintali, Kijiji cha Msamba Kata ya Ninde, Kijiji cha Kisambara Kata ya Ninde, Kijiji cha Lupata Kata ya Wampembe, Kijiji cha Izinga Kata ya Wampembe na Kijiji cha Mlalambo Kata ya Kizumbi.

Mheshimiwa Spika, Serikali ijenge magati ya meli katika vituo vya Namansi (Kijiji), Kijiji cha Ninde, Kijiji cha Msamba na bandari katika Mji mdogo wa Wampembe. Mji huu una biashara za kutosha na wasafiri wengi. Hali ilivyo inapokuja meli ni hatari kwa wasafiri na matukio kadhaa yanatokea.

Mheshimiwa Spika, nashauri Bandari ya Wampembe na barabara toka Sumbawanga hadi Wampembe ikijengwa ni rahisi kupata soko la nafaka ya mahindi Kongo Kusini.

Mheshimiwa Spika, nawasilisha.