Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, nianze na kumpongeza Waziri Mheshimiwa Eng. Kamwelwe, Manaibu Mawaziri Mheshimiwa Kwandikwa, Mheshimiwa Eng. Nditiye, Makatibu Wakuu na Watendaji wa taasisi zote kwa kazi nzuri sana zilizofanywa na kwa kuwasilisha hotuba hii ya bajeti.

Mheshimiwa Spika, naomba nichangie yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza ni kuhusu ujenzi wa viwanja vya ndege. Naishukuru sana Serikali hii ya Awamu ya Tano kwa ahadi ya ujenzi wa viwanja kikiwepo kiwanja cha Nduli Iringa. Nilikuwa naomba Serikali ijitahidi pia kutoa fidia kwa wakati kwa wananchi walioguswa na upanuzi wa kiwanja hicho.

Mheshimiwa Spika, lingine ni kuhusu Shirika la Ndege ATCL. Niungane na wote walioipongeza Serikali kwa ununuzi wa ndege sita. Napongeza pia kwa kuanzisha mfuko wa ndege katika kiwanja chetu cha Iringa, tunaamini sasa hata uchumi wetu kupitia utalii utaongezeka.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali iangalie uwezekano wa kuwa na connection ya kiwanja cha Dodoma angalau kuwa na miruko mfano Mwanza – Dodoma, Mbeya – Iringa, Dodoma – Songea, Dodoma – Dar es Salaam ili kuwe na urahisi wa Makao Makuu kufikika kwa urahisi na abiria ni wengi. Vilevile bei za nauli za ndege ziangaliwe ili abiria wapande wengi.

Mheshimiwa Spika, Sekta hii ya Ujenzi inafanya kazi nzuri sana hapa nchini. Napongeza sana kazi nzuri ya ujenzi wa barabara nchini ikiwepo na mkoa wetu wa Iringa. Katika Mkoa wa Iringa naomba Serikali iangalie na kujenga barabara ya mchepuo itakayosaidia kuchepusha magari makubwa sana kupitia katikati ya mji.

Mheshimiwa Spika, changamoto ya magari makubwa kupita katikati ya mji, kwanza yanaweza kusababisha ajali na hatari kubwa mno. Barabara ni finyu na kuna maduka hoteli na biashara ambazo zinafanya wananchi kuegesha magari na vyombo vya moto katika barabara hiyo. Pia changamoto ni kwamba wafanyabiashara wanashindwa kufanya biashara. Ni lini sasa barabara hiyo ya mchepuo itajengwa ili kuchepusha hayo magari kupita katikati ya Mji wa Iringa?

Mheshimiwa Spika, barabara ya Dodoma – Iringa, ukipita katika kona za Nyangoro, kuna maporomoko ya mawe na wakati wa mvua yanaongezeka. Nimeshauliza sana maswali kuhusiana na changamoto hiyo: Je, ni mkakati gani unawekwa ili kuondoa changamoto hiyo?

Mheshimiwa Spika, lingine ni ujenzi wa reli. Naipongeza sana Serikali kwa kazi kubwa inayofanywa ya kwa ujenzi wa reli hiyo. Ukikamilika utasaidia hata uharibifu wa barabara zetu ambazo zinaharibika kwa kubeba mizigo mizito. Ujenzi huo mpaka sasa umefikia asilimia 50 phase one Dar es Salaam – Morogoro. Mradi huu ukikamilika, utaleta ajira 10,000,000. Ni kazi nzuri sana.

Mheshimiwa Spika, nawapongeza kwa maboresho makubwa mbalimbali ya sheria na elimu kwa bodaboda na bajaji. Pongezi kwa mtambo wa VTS, umesaidia kupunguza ajali barabarani. Changamoto kubwa ni abiria, wakipata ajali wanapata taabu sana. Ni lini Serikali italeta sheria ya kuweka miundombinu rafiki kwa watu wenye ulemavu?

Mheshimiwa Spika, TTCL wanafanya kazi nzuri sana. Je, yale madeni wanayodai katika taasisi za Serikali watalipwa kwa utaratibu gani?

Mheshimiwa Spika, UCSAF inafanya kazi nzuri sana, maeneo mengi yameweza kupata mawasiliano, lakini kuna maeneo bado hayajapata mawasiliano. Kwa mfano, Mafinga ni Kata ya Ideta, Ihowanza – Ipimo – Ihowasa – Kilolo – Kata ya Ihimbo.