Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. Mheshimiwa Waziri pamoja na Manaibu Waziri nawapongeza kwa kazi nzuri mnayoifanya. Nashukuru kwa miradi inayoendelea kujengwa Airport ya Mwanza, ujenzi wa jumba la wasafiri ufanyike haraka kuondoa adha ya wasafiri iliyopo kwa sasa.

Mheshimiwa Spika, usafiri wa ndege Dodoma – Mwanza ni vyema ukaanza kutokana na ukweli usiofichika kuwa Kanda ya Ziwa ina abiria wengi sana wanaotumia usafiri wa anga. Nashukuru nimeona fedha imetengwa kwa ajili ya fidia kwa wananchi wanaotakiwa kuondolewa eneo la viwanja. Ombi langu ni kwamba zoezi lisichukue muda mrefu ili kuondoa kero iliyopo kwa sasa.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri nimeona fedha kidogo zimetengwa katika baadhi ya barabara. Ombi langu ni kwamba barabara ya Nyakato Veta – Igombe TX kilomita 18 ina miaka mitatu; inajengwa kila mwaka kilomita moja. Naomba angalau ikamilishwe ili kuondoa mgongamano. Aidha, barabara ya Airport – Kayenze – Nyanguge Kilomita 45 ijengwe kwa kiwango cha lami ili kurahisisha wasafiri wanaoshuka uwanja wa ndege waendao Musoma waweze kutumia barabara hii badala ya kupita mjini ambako msongamano unakuwa mkubwa sana.

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa kivuko cha Kayenze – Baze unaendelea vizuri isipokuwa wasiwasi wangu ujenzi wa maegesho ya kivuko bado hawajaanza kujenga. Naomba angalau kivuko kinapokamilika kujengwa kiende sambamba na ujenzi na ukamilishaji wa maegesho hayo.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Naibu Waziri wa Ujenzi alitembelea Jimboni na kujionea adha kubwa ya wananchi wa Kigala Kata ya Buswelu kuwa na korongo kubwa ambalo limekuwa mto, limekosa daraja na tayari watoto walishachukuliwa na maji eneo hilo. Naomba ujenzi wa daraja hilo ufanyike.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Naibu Waziri wa Mawasiliano alitembelea Jimboni tukampeleka maeneo yenye kero ya mawasiliano, hakuna mawasiliano kabisa. Orodha ya maeneo tayari nilishakabidhi. Naomba utekelezaji ufanyike ili kuondoa adha ya mawasiliano. Ahsante.