Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Spika, barabara ya Mafinga – Mgololo, barabara ya Mgololo – Mtwango, barabara ya Kasanga – Mtambula – Nyigo ni za muhimu sana katika kuinua uchumi kwa wananchi wa Mufindi. Kuna viwanda vya Chai, Mbao na Karatasi (MPM). Naomba Serikali ianze kujenga kiwango cha lami ili ziweze kupitika kwa mwaka mzima.

Mheshimiwa Spika, pia Serikali isimamie ujenzi wa barabara za vijijini ambazo zinatengenezwa na Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA). Barabara ya Maguvani, Mtambale, Kilolo imeharibika sana wananchi wanashindwa kusafirisha mazao yao. Barabara ya Nyanyembe hadi Idunda, barabara ya Malangali hadi Idunda, barabara ya Sawala hadi Iyegeya, barabara ya Maduma hadi Makugali zipo chini ya TARURA, zimeharibika sana. Naomba Serikali itengeneze barabara hii ili wananchi waweze kusafirisha mizigo yao, pia kurahisisha shughuli zao za kila siku.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali ijenge minara katika Kata ya Idete, Ihowanza, Idunda na Kiyowela. Maeneo haya hakuna mawasiliano kabisa, wananchi wanashindwa kupata mawasiliano kiurahisi.

Mhesimiwa Spika, ahsante. Naunga mkono hoja.