Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Sonia Jumaa Magogo

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. SONIA J. MAGOGO: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa, nianze kwa kuipongeza Wizara kwa nia ya kifufua reli yetu ya Tanga Moshi ambayo ni mwokozi mkubwa sana kwa wananchi wa kanda nzima ya Kaskazini, kwani kwenye suala la usafirishaji mizigo na imeepusha barabara yetu kuharibika mara kwa mara kutokana na mizigo mingi kupita kwa njia ya barabara. Tunaomba mradi huu uwekewe mkazo.

Mheshimiwa Spika, kwa upande mwingine, naiomba Wizara ione umuhimu wa kupanua barabara ya Dodoma inayoenda Dar es Salaam, maana kwa sasa hasa wakazi wa njia hiyo wameshaanza kukumbana na tatizo la foleni hasa kipindi cha jioni na asubuhi.

Mheshimiwa Spika, pia bado matumizi mabaya ya mitandao yanaendelea. Watu wamekuwa wakitapeliwa na hata kutuma vitu visivyofaa kwa jamii yetu na hivyo kupelekea mmomonyoko wa maadili kwa vitendo vya ukatili. Naiomba Wizara itoe adhabu kali na ziwe hadharani ili watu waogope kutenda mambo yasiyofaa. Anayeadhibiwa itangazwe na wengine wasikie waogope na wao.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri tunaomba ukarabati ujenzi wa barabara ya Tanga – Pangani kwa kiwango cha lami. Barabara hii imekuwa ni kero ya muda mrefu sana.

Mheshimiwa Spika, pia barabara ya Bagamoyo – Msata, matuta yamezidi, yapunguzwe kama zilivyo barabara za highway nyingine.

Mheshimiwa Spika, Bandari ya Tanga vitendea kazi vyake ni chakavu sana na ni bandari muhimu sana kwa ustawi wa uchumi wa nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, pia kuliko mizigo kulundikana bandari ya Dar es Salaam, Bandari za Tanga na Mtwara ziimarishwe na mizigo igawanywe kikanda ili kuzijengea uwezo Bandari za Tanga na Mtwara na kupunguza mlundikano sehemu moja.