Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja, nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu na Watendaji wote wa Wizara.

Mheshimiwa Spika, naomba kuzungumzia ujenzi wa barabara ya Kigoma – Nyakanazi. Barabara hii imechukua muda mrefu sana lakini mpaka leo haijakamilika. Nomba Serikali iweze kusimamia ili iweze kukamilika.

Mheshimiwa Spika, kipo kipande cha kutoka Uvinza – Malagalasi, nacho ni tatizo. Tunaomba kipande hiki nacho kiweze kujengwa. Kipo kipande cha Chagu - Kazilambura nacho tunaomba kiweze kujengwa ili wananchi waweze kuondokana na adha ya usafiri.

Mheshimiwa Spika, mwisho, naomba nishukuru Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuweza kukubali barabara ya kutoka Kabingo- Kibundo- Kasulu - Bulingwe kujengwa kwa lami kupitia fedha za AfDB.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, nashukuru sana na naunga mkono hoja.