Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Spika, uendeshaji wa ndege nchini. Serikali iliagiza ndege kubwa (Dreamliner) iko wapi? Mbona hatuoni ikifanya kazi? Inanunuliwa ndege ya maonyesho kwa cash money, kodi za wananchi halafu hatuoni ikifanya kazi kwa kuinua uchumi wa nchi kama ilivyoelezwa na Serikali.

Mheshimiwa Spika, zipo taarifa kuwa ndege hiyo imekodishwa Kenya. Kama ndivyo, hayo ndiyo tunayolalamikia kuwa Serikali ina tatizo katika kusimamia na kupanga priorities. Hivi kulikuwa na sababu gani kukimbilia Dreamliner, ku-invest kwenye ndege ambayo return zake haziwezi kuonekana kwa haraka? Ni bora Serikali ingewekeza kwenye project kama za afya, maji na kadhalika, ndege bora ingetumia PPP.

Mheshimiwa Spika, matengenezo ya ndege ndogo tatu (Bombardier) zaidi ya shilingi bilioni 14, hivi kweli ndege zinajiendesha kwa faida? Kwa nini Serikali isingeachia private sector au nchi zenye uzoefu wa biashara za ndege mfano Ethiopia na kadhalika?

Mheshimiwa Spika, SGR, kwa sasa ajira kwa Watanzania ni asilimia 20 na asilimia 80 ni Waturuki. Hiyo siyo sawa, Serikali ilipaswa kuandaa watu wetu kuingia kwenye ajira kabla ya kuanzisha mradi wa SGR. Kazi ambazo ni professional/technical skills zingefanywa na Watanzania kuliko hivi sasa Watanzania wanaishia kwenye kazi ndogo ndogo.