Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, kwanza nawapongeza Mheshimiwa Waziri Kamwelwe na Naibu Mawaziri; Mheshimiwa Kwandikwa na Mheshimiwa Nditiye kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Spika, kuna shida kubwa ya kukosa minara ya mawasiliano Kata za Shitage, Igulungu na Makazi. Naomba minara katika kata hizo.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Tabora – Mrambali – Ishitimulwa - Mhulidede ni muhimu kuwa na lami. Barabara hii muhimu kwani inaunganisha Mikoa ya Shinyanga na Tabora.

Mheshimiwa Spika, pongezi kwa Mamlaka ya Mawasiliano TCRA. TCRA wamefanya kazi kubwa ya kubadili mawasiliano na matangazo ya TV kutoka analojia na kuwa digitali na kuwa moja ya nchi za kwanza Barani Afrika na ya kwanza EAC. Vilevile wanasimamia mgawanyo wa masafa (frequency monitoring) na ugawaji bora wa leseni za redio na televisheni. TCRA wamefanya kazi kwa weledi sana kusimamia mashirika ya huduma za simu na kuhakikisha wanalipa kodi za Serikali kwa kutumia mtambo wa TTMS.

Mheshimiwa Spika, natanguliza shukrani.