Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, nianze na kuunga mkono hoja iliyopo mbele yetu.

Mheshimiwa Spika, niipongeze Serikali kwa namna ambavyo imeimarisha mitandao ya kiuchumi katika ujenzi wa barabara, madaraja, gati, reli, viwanja vya ndege na bandari. Uwekezaji huu kwenye miundombinu itafanya wawekezaji/uwekezaji kukua kwa kasi na kuongeza mapato ya nchi.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali kufuatilia ukarabati wa barabara za lami unaondelea. Wahandisi wahakikishe wanawashauri wakandarasi kuweka viraka vya lami vinavyofanana na uhalisia wa lami ya zamani. Sasa hivi barabara zetu ziko kama zimechorwa rangi, viraka vyeusi na lami yenyewe nyeupe. Sura ya barabara inaonekana kama ni michoro ya rangi. Taifa letu ni kubwa, nchi yetu tuipe heshima na kuiweka katika sura nzuri inayopendeza.

Mheshimiwa Spika, ahsante, naunga mkono hoja.