Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na napenda kuzungumzia kuhusu ujenzi wa barabara kama Serikali ilivyosema kupunguza msongamano katika jiji la Dar es Salaam nimejaribu kujenga barabara, lakini sasa barabara hizo ambazo zinatokea Ardhi - Makongo - Goba, mpaka kufika Kimara na Mbezi kwa kweli kwenye kitabu imeeleza kwamba barabara ya kutoka Ardhi mpaka Makongo tayari imeshakamilika kwa kiwango cha lami. Napenda kuiarifu Serikali kwamba barabara hii bado haijakamilika kwa kiwango cha lami, bado barabara hii ni changarawe kutoka Ardhi hadi Makongo, kwa hiyo naiomba Serikali ihakikishe hizi kilometa nne zinazotoka Ardhi mpaka Makongo zijengwe katika kiwango cha lami ili kupunguza msongamano kwa sababu eneo la kutoka Ardhi mpaka Makongo kuna kuwa na msongamano na magari kutokana na mashimo mashimo.

Mheshimiwa Spika, nikizungumzia kuhusu barabara ya Tanga - Pangani, Tanga - Pangani siku zote tunaambiwa itajengwa kwa kiwango cha lami, lakini hapa sioni, sasa hivi ninaona kwenye kitabu imeandikwa kwamba tutajengwa kiwango cha changarawe kuanzia Mabanda ya Papa hadi Boza Buyuni, sasa Mabanda ya Papa pale ni katikati ya jiji pale, kuna lami mpaka sehemu ya Mwang’ombe ambayo ni kilometa nne kutoka Mabanda ya Papa, kwa hiyo, pale pana lami, changarawe inaanzia pale Mabanda ya Papa mpaka inafika huko Boza Buyuni. Sasa Serikali iangalie uwezekano wa kuifanya barabara ile iwe katika kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenykiti, na kwa taarifa yenu ni kwamba sasa hivi mvua zinazonyesha barabara kutoka Pangani mpaka Tanga haipitiki tena, inabidi sasa hivi wapitie eneo jingine linaloitwa Tongoni, wapiti Tongoni waende Lumbwa waingie Kisima Tui - Pongwe ndiyo warudi tena Tanga kwa sababu kuna daraja linaitwa Neema limearibika, gari haziwezi kupita. Kwa hiyo, tunaiomba Serikali iangalie uwezekano wa hizi barabara ikamilike kwa kiwango cha lami badala ya kutengeneza tena changarawe maana yake hapa inaonesha kuwa barabara itawekwa changarawe kuanzia Mabanda Papa hadi Buyuni Boza.

Mheshimiwa Spika, vilevile napenda kuzungumzia kuhusu mabasi haya ya mwendokasi. Mabasi ya mwendokasi yametusaidia sana lakini yard ya mwendokasi kwa kweli inasikitisha. Imejengwa mahali ambapo mvua zikinyesha panajaa maji kiasi cha kuharibu miundombinu yote. Kwa hiyo, Serikali iangalie uwezekano wa kujenga tena upya na kufanya drainage system ili maji yaweze kupita chini na ile yard ikaweza kutumika au vinginevyo ile yard ya mwendokasi ihamishwe pale iwekwe mahali pengine, kwa sababu maji pale jangwani yanajaa kiasi cha kuyafanya mabasi tena hayafanyi kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikizungumzia kuhusu reli ya Tanga hadi Arusha, kwa kweli reli hiyo imeshaanzwa kutengenezwa Tanga hadi Same. Cha kusikitisha ile reli pia inatakiwa ifanyiwe usafi. Kwa sababu kuna nyasi zimeota. Sasa mtu mwingine anaweza kung’oa reli, bila mtu kujua reli pale imeng’olewa. Kwa hiyo, Serikali ihakikishe kwamba maeneo yale ambayo tayari yameshatengenezwa na ile reli vile vile inakuwa safi, inalimiwa vizuri ili kama kutakuwa na uharibifu wowote utakaotokea inaweza ikajua.

Mheshimiwa Spika, mwisho, napenda kuzungumzia kuhusu viwanja vya ndege. Kwa kweli Serikali inajitahidi kujenga viwanja mbalimbali vya ndege lakini tatizo linakuja, kuna baadhi ya viwanja vya ndege vinakosa taa na kusababisha usiku ndege haziwezi kutua. Kwa hiyo, tunaiomba Serikali katika viwanja vyote vile ambavyo havina taa za ndege ihakikishe taa zinawekwa ili kuwezesha ndege kutua wakati wa usiku.

Mheshimiwa Spika, mwisho...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)