Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na mimi nashukuru kwa kunipa dakika tano nitajaribu kukimbia kimbia.

Mheshimiwa Spika, ahsante niipongeze Wizara kwa kazi kubwa wanaoifanya katika kuhakikisha kwamba miundombinu ya nchi yetu inaboreshwa.

Mheshimiwa Spika, naomba nianzie jimboni kwangu ambako kwanza ningependa suala la barabara ya Mtwara - Msimbati - Madimba - Kilambo ambazo ni barabara zinazounganisha nchi yaani Tanzania na Mozambique ambayo ni sera yetu kuhakikisha kwamba barabara zinazounganisha nchi zinajengwa kwa kiwango cha lami, Mheshimiwa Waziri naomba utakapokuja kunijibu basi uniambie imefikia wapi suala la kujenga barabara ya Mtwara - Msimbati - Madimba - Kilambo kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, pia kuna suala la barabara ya kutoka Hiari -Nanguruwe ambayo ni mchepuko, sasa hivi kutokana na kiwanda cha saruji ambacho ni kikubwa sana magari yote yanayokwenda Newala hayapiti tena Mtwara yanatumia barabara hii tumeiomba Serikali, nimekuja kwako Mheshimiwa Waziri nimezungumza na Meneja wa TANROADS kuomba barabara hii ichukuliwe na Wizara kwa sababu inapitisha malori makubwa ambapo TARURA peke yake hawawezi kuijenga barabara hii ipasavyo.

Mheshimiwa Spika, katika Halmashauri yangu tulikuwa tunajenga barabara kwa kiwango cha lami kutoka Kivukoni pale Msemo kwenda Msanga Mkuu, lakini barabara hii imekuwa na changamoto kubwa sana watu wa bandari wa Mtwara hawataki barabara ipite katika maeneo yao, sasa maeneo yote hata Dar es Salaam kuna barabara ambazo zinapita ndani ya eneo ya bandari na kule Msanga Mkuu ni lazima upite katika bandari ndipo uweze kufika katika vijiji vyetu.

Mheshimiwa Spika, naomba Mheshimiwa Waziri aingilie kati kwa sababu barabara hii ilikuwa inajengwa sasa hivi imesimama kwa eti tu kwamba hatuwezi kujenga barabara ya lami kupita eneo la bandari eneo ambalo hata kuendelezwa bado alijaendelezwa. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri naomba uingilie kati suala hilo.

Mheshimiwa Spika, tunayo barabara yetu ya kutoka Mpapura kwenda Kitere mpaka Mkwichi kule Mtama, naomba hii barabara inaunganisha mikoa, Mkoa wa Lindi na Mkoa wa Mtwara kama kawaida tunaomba barabara hii ijengwe kwa kiwango cha lami kwa sababu ndiyo sera kuziunganisha kwa kiwango cha lami barabara zote ambazo zinaunganisha mikoa.

Mheshimiwa Spika, na mimi niungane na wenzangu kuzungumzia suala la Bandari ya Bagamoyo, hata wenzetu China walivyotaka kuendeleza nchi yao, walivyotaka kuanzisha maeneo ya special economic zone walianzia na China ya Mashariki ambako ndiko ambako wanapakana na bahari. Sasa kuanzia Djibouti mpaka tunafika kule South Africa, sisi hapa tulikuwa na nafasi kubwa sana ya kuwa na bandari kubwa ambayo itachukuwa meli za four generation ambazo zingeweza kuleta mizigo baada ya kufika pale ile mizigo sasa ndiyo ikawa inaenda kwenye bandari zingine za Beira, Mombasa, Dar es Salaam na maeneo mengine.

Mheshimiwa Spika, niiombe Serikali yetu suala hili waliangalie kwa mtizamo mpana zaidi na hasa wakisikiliza na Wabunge michango yao pamoja na mchango wako.

Mheshimiwa Spika, na suala la mwisho ni suala la Reli kutoka Mtwara kwenda Mbambabay na matawi la kwenda Liganga na Mchuchuma. Tunategemea kuchimba chuma, kuchimba makaa ya mawe na alivyokuja Waziri wa Ujenzi alisema kuna tender ya kupeleka...

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.