Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii.

Mheshimiwa Spika, bila kupoteza muda, dakika tano ni chache sana, naomba nianze na suala la barabara ya Mogitu – Haydom – Sibiti. Mheshimiwa Rais aliahidi kwamba itaiwekwa barabara hii lami kwa sababu tuna Hospitali ya Rufaa kule na watu wengi wa maeneo ya Hanang, Mkalama na hata Sibiti yenyewe wanakuja pale Haydom kupata huduma ya afya.

Mheshimiwa Spika, suala la pili, kuna maeneo ambayo wakati mvua ya El-Nino iliponyesha, makorongo makubwa yalitokea na yakitenganisha shule na watoto au zahanati na wagonjwa. Kwa hiyo, naomba wasiiachie Halmashauri tu, Wizara hii ya Ujezi nayo isaidie na namwambia Waziri kila siku.

Mheshimiwa Spika, jambo la tatu, naomba ni-declare interest kwamba aliyesaini mkataba ule kuhusu Bandari ya Bagamoyo ni mimi wakati nikiwa Waziri wa Uwekezaji. Nataka niwaambie tulifanya hivyo kwa sababu ilionekana Afrika nzima Ukanda wa Pwani the best place ya kuweka bandari ni Bagamoyo lakini Bagamoyo si bandari tu, Bagamoyo ni Economic Special Zone ambapo kutakuwa na viwanda na miradi mingine mingi ambayo itainua uchumi wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninaomba sana na mimi nisingesemea, mimi natoka Hanang huko hakuna bandari, lakini naisemea Bagamoyo kwa sababu kwa kweli ni mahali ambapo itasaidia sana na hii SGR itumike vizuri kuleta economic change kwenye Tanzania yetu na kwa kweli naombeni sana muangalie hilo na sisi Wabunge nimeshukuru sana Spika mwenyewe alivyosema na sisi wote tuwe pamoja, lakini sidhani kama hii Serikali wala inakataa, ina sababu labda kuchelewesha, lakini wajuwe ya kwamba kwa kweli hapa ni mahali ambapo tukipapuuza tunapuuza kukuza uchumi wa nchi hii ulingane na tunachotaka baadaye.

Mheshimiwa Spika, ya mwisho Rufiji si mahali padogo ni mahali pa kubwa, babu yangu mimi alikuwa akipingana sana na wakoloni wakampeleka Rufiji wakamzika huko alipokufa, sasa na mimi nashindwa kwenda kuona lile kaburi la babu yangu, kwa hiyo tumsaidie Mchengerwa na yeye tuone umuhimu wa kuona eneo ambalo ni muhimu sana.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru na ninaunga bajeti hii mkono na nina imani na Serikali hii kwamba wala haina shida na Bagamoyo, lakini wataona umuhimu wake na kutoa kipaumbele, ahsante sana, sana na Mungu akubariki. (Makofi)