Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa dakika hizo.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu utajielekeza kwenye masuala ya infrastructure na hasa Bagamoyo kama ulivyosema wewe na baadhi ya Wabunge.

Mheshimiwa Spika, ombi langu kwako, sasa hivi lazima tuwe na new thinking kwenye economic corridor nchini Tanzania. Bila kuweka new thinking tutaendelea kuwa waoga wa kufanya maamuzi, kutoa ushauri na kuirudisha nyumba hii. Uzalendo haimaanishi kukataa kila kitu, lazima tuwe na calculated risk. Risks hizi zinapimwa na zinaweza zika-work Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ombi langu kwako; negotiating team hii ya Tanzania ipate fursa ya kuja kwenye Bunge lako, ikae na Wabunge wajaribu ku-brainstorm na kusaidia nchi yetu iweze kwenda mbele na hasa kwenye mradi huu wa Bagamoyo. Infrastructure za nchi nyingi sana zimeendeshwa na gold backed currency; deposit ya gold na baadhi ya madini nchini mwetu yanaweza kutumika ku-fund infrastructure katika nchi yetu. Naomba wataalam wa nchi yetu watazame suala la gold backed currency ili kuweza kujenga taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napongeza watendaji wa Serikali, nampongeza Waziri, naipongeza Wizara hii kwa kazi nzuri wanayoifanya. Mchango wangu ulikuwa ni huo tu, Bunge lipate nafasi kukaa na team inayo-negotiate Bandari ya Bagamoyo ili tupeane taarifa mbalimbali na tu-move this country forward. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naunga mkono hoja. (Makofi)