Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa na vilevile nikushukuru kwa dhati kabisa kwa maamuzi uliyofanya ya kuchangia kuhusu Bagamoyo. Ni jambo muhimu sana. Investiment ya Special Economic Zone ya Bagamoyo ilikuwa inatuletea inflow ya 10 billion US Dollar kwenye uchumi wetu na ni jambo ambalo ni vizuri Serikali wakati Waziri anakuja kufanya wind-up watueleze kinagaubaga kwa nini mradi huu unasimama?

Mheshimiwa Spika, nataka niongelee SGR. Kumekuwa na mjadala mkubwa sana na last week kulikuwa kuna mjadala mkubwa hapa ndani ya Bunge kwamba mradi wetu wa SGR kwa nini hauonekani kama unatuletea impact na mzunguko wa fedha kwenye uchumi?

Mheshimiwa Spika, nilitaka nije niombe kwamba wakati Waziri anakuja kufanya wind-up na hasa Waziri wa Fedha, the financing model ya SGR ya Dar es Salaam – Makutupora: Je, itaendelea kuwa hiyo hiyo model ya financing kutoka Makutupora kwenda Tabora; Tabora – Mwanza, Tabora – Kigoma, Uvinza – Msongati? Kwa nini nasema hivyo?

Mheshimiwa Spika, the financing model tunayofanya, which is very good, mimi sipingani nayo katika hatua hii ya awali, kwamba tunatumia fedha zetu kujenga reli hii. Sioni kama tukiendelea hivi mpaka mwisho itatusaidia ndani ya uchumi wetu. Kwa sababu tunakusanya shilingi na tunapomlipa huyu Mkandarasi ni ratio ya 65:35. 35% ya fedha zake analipwa kwa shilingi. 65% analipwa kwa dola.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kinachotokea ni kwamba shilingi inakuwa converted into dollar, halafu dola analipwa Yapi nje, halafu Yapi anarudisha ndani dola ai- convert into shilling kuwalipa local contractors. Kinachotokea ile process ya kuhamisha shilingi kwenda kwenye dola there is a cost, kwa sababu we are losing money in that process. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili kuna tatizo kubwa la Mkandarasi wa Yapi kulipa local contractors. Hili nalo ni tatizo, ni vizuri Wizara ikaliangalia. Hili ni jambo muhimu sana. Tuangalie financial model ya ku-finance mradi wa SGR kuanzia Makutupora kwenda mbele ubadilike. Bila hivyo, uchumi utaendelea ku-suffocate.

Mheshimiwa Spika, sitaki kujadili takwimu za IMF, hizo ni kazi za zao, lakini ninachotaka niwaulize, ukiangalia trend, toka mwaka 2014 construction sector in general, 2014/2015 ili-grow by 16.8%, leo ina-grow katika wastani wa asilimia 13. What is the problem? Shida ni nini wakati tunapeleka fedha nyingi sana za development budget kwenye construction sector? Kuna nini? Hili ni jambo ambalo lazima tujiulize Serikalini.

Mheshimiwa Spika, tuangalie 2014 to date, average growth yetu ya GDP ni asilimia sita point something, imekuwa namna hiyo mpaka leo. Kuna nini wakati tunapeleka fedha nyingi sana kwenye construction? Hili ni jambo moja.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ambalo nataka nitoe ushauri, Mheshimiwa Waziri Kamwelwe, TRC wako pale, washauriane hili. Sisi tunajenga SGR kwenda Mwanza. Our cash cow kwenye reli ni mizigo na ni nchi ya Uganda, Congo, Zambia na Malawi.

Mheshimiwa Spika, nashauri, TAZARA inasuasua, TRC ikodi infrastructure ya TAZARA halafu wanunue wagon kwa ajili ya kuhudumia Zambia na Malawi. Wakati huo tutakuwa tunalipa fee kwa kutumia infrastructure hiyo, TRC wanunue mabehewa na vichwa ambavyo vinaweza kupita kwenye reli ya TAZARA ili wabebe mizigo ya Zambia na Malawi, tutapata revenue.

Mheshimiwa Spika, la pili, leo sisi tunataka kumpelekea huduma Mganda ambaye ana-constitute aslimia 30 ya mzigo wetu. Tujenge kipande cha Port Bell kwenda Kampala ambacho ni kilometa 11, tuweke meli kubwa, mzigo utoke Dar es Salaam mpaka Mwanza, uingie kwenye hiyo meli kubwa ibebe mizigo tupeleke Port Bell. Tutakuwa na competitive age. Kinachotokea, tunaye-compete naye leo ambaye ni Mombasa anamjengea bandari kavu Mganda, Naivasha ili kupunguza distance iliyoko ambayo sisi kwetu ni competitive age. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la tatu, kwenda Msongati ni kilometa 200, ninawashauri achacheni na reli ya kwenda Rwanda, wekeni fedha kujenga Msongati kuja Uvinza. Tujenge kwa SGR. Tukijenga kwa SGR kutoka Msongati kuja Uvinza mzigo utabebwa kutoka Msongati kuja Uvinza kwa Standard Gauge. Kutokea pale tutatumia meter gauge kuja Dar es Salaam. Kwa hiyo, tutaanza kupata fedha kabla ya reli kufika Mwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la nne, we only have 30 kilometers kuhudumia Eastern Congo ambayo ina population ya 22 million people. Ushauri, shaurianeni na Serikali ya Congo tufanye joint effort tujenge gati upande wa Congo tuweze kubeba mizigo kutokea Kigoma kwenye meli kubwa tuvushe kwenda Kalemii ili tuanze kuwahudumia hawa wakati tunasubiri ku-generate revenue. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, this is a question of where to get money. Kwa nini nasema hivi? Leo Mozambique wamejenga reli kwenda Zambia, ili…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Bahati mbaya dakika saba ndiyo hizo.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, naomba Serikali waangalie maeneo ambayo wanaweza kupata fedha. Ahsante, naunga mkono hoja. (Makofi)