Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Zubeda Hassan Sakuru

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ZUBEDA H. SAKURU: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kushukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia lakini kabla ya kuanza kuchangia ningependa kushukuru chama changu cha Demokrasia na Maendeleo kwa kunipa nafasi ya kuwa mwakilishi wa Mkoa wa Ruvuma kupitia Baraza la Wanawake wa CHADEMA.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia kabla sijachangia ningependa kupongeza hotuba ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani ambayo imekuja na mawazo mbadala na naamini kwamba Waziri ukiwa makini utaweza kuyachukua mawazo yetu kwa sababu yanaelezea viini vya matatizo lakini pia yanaelezea ni wapi tunaweza kulipeleka Taifa letu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu ya Tanzania iko rehani. Leo tunapozungumza, tunazungumza juu ya mtoto wa Kitanzania ambaye anashindwa kushindana katika soko la ajira katika dunia hii. Kwenye dunia ambayo tunaendana na kasi kubwa ya mabadiliko ya kiuchumi na teknolojia, mtoto wa Tanzania leo anajifundisha kuhusu World War One lakini application yake katika maisha ya kawaida hatuyaoni. Sidhani kama Marekani, nchi zilizoendelea leo wanajifunza kuhusu Majimaji War na bado wana mapinduzi katika uchumi wa viwanda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapozungumzia kuhusu mtoto wa Kitanzania katika ushindani wa soko la ajira, tunampeleka wapi mtoto wa Kitanzania ambaye leo atika mfumo wa elimu kuanzia primary education mpaka secondary education anasoma kitu kile kile lakini kwa replication ya utofauti wa lugha! Kuanzia darasa la tatu mpaka darasa la saba binti wa Kitanzania, kijana wa Kitanzania anasoma kuhusu sayansi kwa lugha ya kiswahili, akienda kusoma form one mpaka form four anaenda kusoma the same thing katika lugha ya kiingereza. Tunaenda mbele au tunarudi nyuma?(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, bado tuna changamoto kubwa ya kuweza kushindana na soko la ajira katika Afrika Mashariki, na nioneshe masikitiko yangu makubwa kwamba kati ya vitu ambavyo Tanzania imeviweka rehani kwa mfano tukizungumzia suala zima la elimu ni pamoja na kubadilishwa kwa mitaala kwa kauli za Mawaziri. (Makofi)
Leo Taifa letu linaendeshwa kutokana na kauli za Mawaziri au vision ya Waziri badala ya vision ya Kitaifa ya mtaala wa elimu! Akija mmoja leo akifikiria kwamba sayansi ni muhimu kwa watoto wa Kitanzania, basi wote tunasomeshwa sayansi, akija mwingine akiamini kwamba biashara ni muhimu kwa waototo wa Kitanzania wote tnasomeshwa biashara, tunaelekea wapi kama Taifa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nabado tujue kwamba na nashukuru kwamba Waziri Mkuu katika hotuba yake aliyoitoa Aprili, 2016 alizungumzia kuhusu kutoajirika kwa kijana wa Kitanzania kwa kushindwa kupata elimu na ujuzi wa kuweza kujiajiri na kuajiriwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ipo haja ya sisi kama Tanzania, set aside our political differences, kuwa na mpango wa Kitaifa utakaoweza ku-match gap kati ya mahitaji ya soko la ajira na kile tunachokizalisha. Leo hii ukimchukua mtotowa Kitanzania kwenda kushindana na mtoto Jumuiya tu ya Afrika Mashariki, mtoto wa Kenya, mtoto wa Kitanzania anakaa wapi? Mhitimu wa Kitanzania anakaa wapi? Tunacheza pata potea kwenye elimu na tumewaweka watoto wa maskini katika ombwe wasijue watafanya nini wanapohitimu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii nasikitika sana Serikali inapokuja na hoja ya kuwa na ada elekezi. Unawekaje ada elekezi pale ambapo umeshindwa kuboresha miundombinu ya shule za Serikali? Na niseme tu mimi ni tunda au uzao la shule za Serikali, nimesoma all government schools, lakini shule nilizosoma leo ukiangalia matokeo yake na quality of the output they put in the market is a mess, is a shame. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapozungumzia kuhusu masuala ya kutoa ada elekezi lazima tuji-reflect katika matendo yetu, miundombinu ambayo tumeiweka katika shule za Serikali ni rafiki? Leo mnazungumzia kuhusu mimba za viherehere na nashukuru sana baadhi ya Wabunge wa upande wa Kambi ya CCM wamezungumzia kuhusu mimba za utotoni, lakini Rais wa Awamu ya Nne aliyekuwa na dhamana alisema ni mimba za viherehere, ni kauli mbaya ambayo haijawahi kutolewa na Mkuu wa Nchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua kabisa changamoto ya watoto wanaotoka vijijini imetokana na ubovu wa miundombinu, umbali wa shule, lakini pia kutokuwa na miundombinu rafiki kwao. Leo hii tuna wanafunzi ambao wamepewa mimba na walimu wa shule za msingi, how do we place them katika market? Nafikiri Waziri kwa sababu wewe ni mwanamke na tupo katika zama za kuweza ku-value mchango wa mtoto wa kike katika kujenga uchumi na kujitegemea, basi naamini kwamba leo utatoa agizo la kufuta the ban ya watoto wa shule wanaopata mimba kutorudi shuleni. (Makofi)
Kuna kitu ambacho kinanifurahisha sana. Wakati ukiwa Mkurugenzi wa Baraza la Mitihani la Taifa, sorry! Mheshimiwa Waziri ulitoa picha mwanafunzi amechora zombie na akachekwa, lakini je, Tanzania tuna wachoraji wa kutosha kujivunia? Katika mitaala yetu, tuna mitaala ambayo inaweza ku-accomadate fine and performing arts? Au sisi tunachagua tu baadhi ya career? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, huyo kijana aliyechora zombie kama angepewa elimu ya ziada ya kuweza kujifunza fine and performing arts, si ajabu alivyochora zombie angepata A. leo hii anawekewa failure kwa sababu ameshindwa ku-accommodate masomo. Na mimi Mheshimiwa Waziri nikuambie Mheshimiwa Mwenyekiti aniruhusu, ni kati ya wanafunzi ambao waliweka determination na kuacha kile ambacho niliambiwa nisome. Leo katika Tanzania watoto wengi wanasoma si vile ambavyo wao wanataka bali mfumo unachotaka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazalisha madaktari wengi, juzi katika hoja sikuchangia, lakini katika hoja ya Wizara ya Afya kuna wanafunzi wahitimu karibu 1,000 ambao wamesoma udaktari leo hawana kazi, mfumo umewatenga. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie tena kuhusu migogoro inayoendelea katika vyuo vyetu vikuu. Ni dhahiri, shahiri kuna matabaka ya ushiriki wa wanafunzi katika vyuo vikuu kutokana na matabaka ya utofauti wa itikadi zao. Pamoja na kwamba kuna Mbunge aliongea hapa akaelezea kwamba hakuna u-CHADEMA, hakuna u-CCM, tuna ushahidi wa mwanafunzi ambae alikuwa Vice President wa Chuo cha UDOM ambaye amesimamishwa masomo kwa sababu tu ya kushindwa kufanya kazi kama ambavyo management ya chuo ilitaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwanafunzi huyu Rose Machumu alienda mahakamani akafungua shauri na katika shauri lake mahakama iliona kwamba alikuwa na legal stand ya kuwa kiongozi, lakini akapinduliwa. Mapinduzi tu haya ya kawaida tu haya ya kwenye kura za kawaida huku mtaani mnahaha, kwenye vyuo vikuu mnashindwa kushughulikia kwa nini? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niangalie kuna kitabu hiki cha Africa Development Bail Out kimeandikwa na Profesa Norman A. S. King ambaye ni mwanachama wenu. Anaelezea na ame-rank reasons za kwa nini Tanzania hatuendelei. Mojawapo ya changamoto ambazo ni kwa nini Tanzania na mfumo wa elimu hauendelei ni pamoja na kutokuwa na match kati ya uhitaji wa walimu na wanafunzi kitu ambacho ni kweli, lakini kingine anasema poor quality of teachers in primary school yaani walimu wa shule za msingi hawakidhi viwango. Lakini pia anasema lack of housing for teachers, kukosekana kwa malazi kwa ajili ya walimu kumesababisha kuwa na matokeo mabaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bado kuna changamoto nyingine nyingi ambazo shule zinakumbana nazo na leo hii mimi huwa nashangazwa sana, tunasemaje kwamba kuna upungufu wa madarasa, tunashangiliaje kuwa na ongezeko la madarasa nchini kama kiwango cha utoaji wa elimu kiko duni? Tunawezaje kushangilia ongezeko la wanafunzi wanaofaulu wakati kati ya hao wanaofaulu hawajui kusoma na kuandika? Tunawezaje leo kushangilia kuwa na ongezeko la maabara ambazo kimsingi hizo maabara hazitoweza kufanya kazi mpaka sijui bajeti ya mwaka gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaongeleaje kuwa na maendeleo katika sekta ya elimu wakati mwalimu wa Kitanzania hana malipo stahiki wala yenye staha na kumuwezesha kumudu haki zake? Tunazungumzia kwamba kuna mambo mengi ya msingi ambayo yanatakiwa kufanyiwa kazi, kuna kitu ambacho kina-neglect na kuvunja moyo sana na kuvunja moyo sana katika Taifa letu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu wanaitwa Tanzania One, wale vijana waofanya vizuri katika msomo yao, wakishakuja Bungeni, wakipigiwa makofi, wakishapewa zawadi laki moja, laki mbili hatma yao haijulikani. Kwanza nitoe pongezi zangu kwa mwanafunzi Gertrude Clement aliweza kuhutubia UN lakini pia…
MHE. ZUBEDA H. SAKURU: Mheshimiwa Mwenyekiti, siungi mkono hoja.