Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kunipa nafasi niweze kuchangia katika Wizara hii. Kwanza kabisa napenda kumpongea Mheshimiwa Waziri na Manaibu Waziri wake, Makatibu Wakuu na watendaji wote wa Wizara hii kwa utendaji wao mahiri katika Serikali yetu. Lakini napenda nitoe salamu za pongezi kwa Mheshimiwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uamuzi wake wa busara wa kununua ndege sita. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi ni Wabunge tunafika sehemu lazima tuwe wa kweli nchi yetu kwa kukosa ndege ilipwaya. Leo anatoka mtu anasema kwamba ndege hizi hazina faida zina hasara kubwa lazima tuwe wa kweli faida ya ndege huwezi kuiona hivi hivi, kuna mambo hayawezi kuonekana moja kwa moja. Kwanza ndege zinasaidia katika eneo la utoaji wa huduma kwa haraka katika nchi lakini pia ndege itasaidia kutangaza Utalii, pia zinasaidia kutuletea fahari yetu kama Watanzania na sisi tunapoona Twiga wetu wa ATCL anaruka kutoka kwenye nchi yetu kwenda kwenye nchi jirani kama mtanzania na mzalendo kwa kweli unajisikia moyo wako una amani kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia ndege hizo ziteleta fedha zitasaidia katika kuongeza mapato ya Serikali kupitia uwekezaji utakaoendelea kutokana na kutangazwa kwa Utalii na mambo mbalimbali katika nchi za jirani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo napenda tena nimpongeze Mheshimiwa Rais tena wa Jamhuri ya Muungano kwa kuwa Rais wa Watanzania wote bila kujali ametoka katika mkoa gani. Nasema hayo kwa uzalendo mkubwa nikiwa na ushahidi kwa yale yaliyotendeka katika Mkoa wa Dar es Salaam. Katika Mkoa wa Dar es Salaam katika kipindi kifupi kumefanyika miadi ifutayo;

(i) Lilikamilika daraja la Kigamboni,

(ii) Flyover ya TAZARA ya Mfugale,

(iii) Interchange ya Ubungo imeanza,

(iv) Barabara nane Kimara kufika Kibaha mradi huo umeanza,

(v) Ujenzi wa daraja la Mlelakuwa umekamilika,

(vi) Ujenzi wa daraja la Salenda umeanza na uko kwenye hatua nzuri, Kuanza kwa barabara na miundombinu ya mwendokasi kutoka Gerezani, Bendera Tatu mpaka Mbagara Rangitatu. (Makofi)

(vii) Ujenzi wa Uwanja wa ndege wa Kimataifa umekamilika kwa asilimia 90 ,

(viii) Ujenzi wa reli na upanuzi wa bandari gate namba 13 umekamilika bandari ya Dar es Salaam, maboresho makubwa ya barabara katika Mkoa wa Dar es Salaam kupitia mradi wa DMDP kwa kweli yameleta sura nyingine kabisa katika Mkoa wa Dar es Salaam. Hayo yote yametokana na uzalendo wa Mheshimiwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano ambaye yeye kujali nini ni Rais wa Watanzania wote akaona pamoja na kuhama kwa Makao Makuu kutoka Dar es Salaama na kuwa Mji wa kibiashara basi mambo haya yameboreshwa.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kutoa pongezi hizo kwa Serikali sasa naomba nijikite mchango wangu katika ukurasa wa 24 barabara ambazo zimekamilika ziko katika upembuzi yakinifu. Barabara ambayo iko kwenye upembuzi yakinifu ni barabara ya Kibada, Tudwi, Songani, barabara hii kwa kweli yaani ni ya muda mrefu kila wakati ipo kwenye upembuzi wananchi wa kule Tundwi Songani wako katika hali mbaya sana mvua zinaponyesha wanakuwa hawana mawasiliano kabisa. Niiombe Serikali yangu waangalie kwa jicho la huruma wananchi wale wanaokaa Tundwi Songani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia barabara nyingine ambayo ipo kwenye upembuzi na kuanza ni barabara ya Mbagala Rangi Tatu, Kongowe pamoja na daraja la Mzinga. Niiombe Serikali hii barabara ni muhimu sana watu wote wa Kusini lazima wapite kwenye daraja la Mto Mzinga lakini daraja lile sasa hivi limewekwa daraja la muda lile la kijeshi hakuna hata pembezoni sehemu ya kupita watu watu wakiwa kundi hawawezi kuvuka pale. Kwa hiyo, niiombe Serikali waharakishe barabara hii kwa ajili ya watu wanaoelekea katika mikoa ya Kusini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado kuna barabara ya Kongowe, Mji mwema Kivukoni tunaomba barabara hiyo iko kwenye mpango kabisa wa kujengwa kweli barabara hiyo itakapojengwa waangalie jinsi ya kuiongeza upana, barabara sasa ni finyu na mji wa Kigamboni sasa umekuwa tumekuwa na Wilaya mpya ya Kigamboni, kwa hiyo, barabara ile pamoja na kuboreshwa bado waongeze upana wa barabara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna barabara ya Kitunda, Kivule kwenda Chanika Msongola. Barabara hii muda mrefu inajengwa vipande lakini hatuelewi kwa nini Mheshimiwa Waziri nakuomba sana utakaposimama uje unieleze hii barabara ya Kitunda, Kivule kwenda Msongola ina matatizo gani mpaka haiendelezwi? Wananchi wa kule wamechoka. Mbunge ninayetoka Dar es Salaam wameniomba nije nikuombe na utakapomaliza Bunge uende pale ukaeleze wananchi wa kule hivi ni sababu gani zinakwamisha ujenzi huu usiende vizuri? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nije kwenye barabara ya Nzasa, Kilungule, Mwanagati, Buza. Barabara hiyo kila nikisimama hapa Bungeni hebu Mheshimiwa Waziri unionee huruma wananchi wa kule bado kunahitaji daraja la Kilungule kwenda Mparange wananchi wanavuka daraja la miti kama wako kijijini kumbe ni Jiji la Dar es Salaam ile hali haipendezi nikuombe Mheshimiwa Waziri kila siku tunaambiwa pesa iko tayari kila kitu kiko tayari mkandarasi atatangazwa kesho, kesho hii itaisha lini? Naomba sasa barabara hii itekelezwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa nichangie kwenye eneo la bandari, napenda kutoa pongezi kutokana na taarifa kwamba bandari imefanya vizuri, kama inafanya vizuri basi ndio tunavyoomba niombe sasa liko tatizo bandari baada ya mkumbo wa vyeti feki hakuna waajiriwa wengi walitoka, sasa hivi Serikali inawatumia SUMA JKT kuajiri vibarua. Natoka Mbagala lazima nikatishe bandarini kila siku watoto wale wanajaa pale nje wanasubiri kibarua cha shilingi 9000 lakini sasa tuone kibarua kile niiombe Serikali tumuamini kuna Mkurugenzi wa Bandari na ni Mkurugenzi mahili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama ni Mkurugenzi mahili kwa nini hamna maeneo ambaayo mkaangalia jinsi ya kufanya mkataba leo hii anaajiriwa dereva wa kumbeba Mkurugenzi anamtoa Mkurugenzi wadogo wadogo hawa anamtoa Dar es Salaam mpaka Dodoma kutwa analipwa 9000 jamani hivi kweli tuangalie kada za kuiachia SUMA JKT lakini tuangalie sekta nyingine vitu vingine kama vinaangalia basi watu hao wapewe hata mikataba midogo. Mtu yupo daktari pale na yeye anachukuliwa kama kibarua nurse anapewa 9000 kwa kutwa jamani hii kitu hapana lazima tuangalie na level. Kama tunakwenda kuwachukua hawa watu wadogo, vibarua vidogo hivi wa SUMA waende lakini maeneo mengine makubwa basi Mkurugenzi apewe mamlaka ya kuangalia mikataba midogo ili wale watu wafanye kazi yao vizuri wasiwe na tamaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niombe Serikali fungu la CSR linatolewa kwa jamii katika Mamlaka ya Bandari naomba sana nimewaona sisi kama Dar es Salaam hatuna kitu kingine tunawategemea wao niliwaona mara moja wakitoa magodoro shule ya uhuru lakini nawaomba tena waangalie kwa jicho la huruma watoto wenye mahitaji maalum wenye magonjwa ya usonzi wenye usonzi Sinza maalum, Mtoni maalum wale tukiwapa huduma jamani wana mahitaji makubwa Mamlaka ya Bandari kama inaingiza faida basi rudisheni kwa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije sasa kwenye reli nashukuru sana na naipongeza sana Serikali kwa kujenga reli ya standard gauge kwa kweli pale Dar es Salaam tu ukifika pale gerezani imeanza kubadilisha sura ya Jiji. Pia kuna mpango wa reli za mjini Dar es Salaam , reli hizo zitakuwa zikitoka uwanja wa ndege Mbagala, Chamazi, Buguruni, Kibaha, Bunju mpaka Bagamoyo ni jambo jema tunaiombea Serikali mambo haya yaende vizuri ili hii treni iweze kukamilika. (Makofi)

MWENYEKITI: Maliza.

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho naomba barabara ya kutoka Mbuyuni Kawe, kuelekea Mbweni barabara ile iko ufukweni haina taa giza kubwa, wananchi wa kule wanapata shida naunga mkono hoja asilimia 100 ahsante sana. (Makofi)