Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kupata nafasi hii. Kwanza naipongeza Kamati yangu, tumekwenda ziara. Vile vile nampongeza Mheshimiwa Rais, nampongeza pia Mheshimiwa Waziri kwa kufanya kazi nzuri katika Kamati hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumze kuhusu bandari iliyojengwa Tanga, Mtwara na Dar es Salaam. Hiyo yote imeboresha zaidi. Vilevile nampongeza Mheshimiwa Rais kwa kufanya juhudi sana kuhusu barabara. Tulitembea Mbeya na Kamati, tumeona kazi ya barabara imefanyika na watu wananchi wameridhika sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Kamati yangu katika ziara yake tumeona Standard Gauge inakaribia kukamilika kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro. Hata hivyo wamejenga bandari kavu. Kwa hiyo, tunapongeza, ila kwa kuwa container zote zinakaa Dar es Salaam, basi zitakuwa zinakaa katika bandari ile kavu ya kule. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri amechukua hatua nzuri sana katika mambo mbalimbali ya mawasiliano ya barabara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, umenipa nafasi haraka haraka, lakini nilikuwa sijajiaandaa, nilikuwa nimejiandaa kwa jioni, lakini kidogo umenipa nafasi siyo mahala pake, mawasiliano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumze kuhusu bandari iliyojengwa Mtwara. Tulipokwenda Mtwara, tuliona bandari ya zamani ilikuwa ndogo lakini sasa imepanuliwa zaidi. Nimeona hata Bandari ya Dar es Salaam, Kamati tumeambiwa kwamba kunafanyika uboreshaji wa njia ya meli, badala ya kupita meli moja, zitapita meli mbili pamoja. Kwa hiyo, nashukuru kwamba hayo yote yatafanyiwa kazi. Namshukuru sana Mwenyekiti wa Kamati amefanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile Mheshimiwa Rais ameboresha uwanja wa ndege wa Dar es Salam tumeona, amenunua ndege nyingi na wanaleta utalii. Pia ndege itakwenda katika nchi nyingine kama India, China na sehemu nyingine na Iringa hivyo hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kumalizia, namshukuru sana Mheshimiwa Rais wetu, anajitahidi kwa kukusanya pesa na kazi kwa Watanzania wanyonge na wengine wote. Kupitia mabasi ya mwendokasi, watu wamefaidika kwa bei ndogo na tunaingiza mapato chungu nzima, ila tu sasa hivi siku za mvua nashauri yajengwe madaraja kwa sababu tunapata taabu sana kwa kujaa maji barabarani. Hata hivyo...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Haya, ahsante Mheshimiwa.

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, naunga mkono hoja. (Makofi)