Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kunipa fursa hii ili kuweza kuchangia katika Wizara hii ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema ili nami kwa siku ya leo kuweza kuchangia hoja hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitaanza kwa fedha zitolewazo katika Wizara hii ya Uchukuzi, kinachotakikana hapa fedha zifikishwe kwa wakati ili miradi iliyopangwa na Serikali iweze kutekelezeka kwa wakati. Endapo Bunge litapanga bajeti na fedha hazitafika kwa wakati ndiyo chanzo cha miradi mingi kutotekelezeka. Naishauri Serikali ipeleke fedha kwa wakati katika Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ningependa kuzungumzia kuhusu minara ambayo imejengwa katikati ya makazi ya watu hususan katika Mkoa wa Dar es Salaam. Watu wengi wanasema kuwa minara ile ina madhara, wengine wanasema ina mionzi, lakini ningependa kuona sasa Serikali itoe tamko na kutoa hofu kwa wananchi wetu, kwamba ile minara kama ina madhara yoyote au haina madhara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, maana yake watu wengi hutoa maeneo yao katikati ya mji ili kuweza kuweka ile minara ya simu, lakini wengine wanasema ina mionzi lakini bado utafiti haujafanyika. Naomba kama Serikali itakapokuja hapa kujibu itueleze kwamba, je, minara ile ina madhara yote kwa binadamu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tunaona majengo marefu yanajengwa katika Mkoa wetu wa Dar es Salaam, lakini majengo hayo hayana ile fire escape, tumena majengo ya kizamani, wakati mimi nasoma Chuo Kikuu cha Mzumbe, mwaka 1993/95 kuna majengo mabweni ambayo ngazi ambazo ziko nje ya jengo, ambayo hiyo hata ikitokea hatari ya moto watu huweza kukimbia, lakini majengo mengi yanayojengwa katika Mji wetu wa Dar es Salaam, hayaonyeshi kama hatari yoyote ikitokea watu wakimbilie eneo gani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nashauri katika ujenzi unaojengwa sasa hivi, ionyeshe fire escape kwamba watu ikitokea tahadhari yoyote ya moto au chochote watu wanaweza ku, isitokee eneo hilohilo wanaloingilia ndiyo eneo hilohilo wanalotokea ili kuwaondosha madhara zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia napenda kuongelea kuhusu barabara zetu zinazojengwa hivi sasa, barabara nyingi kuu zinazojengwa zina matatizo sidhani kama wakandarasi hao wako competent au vipi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitazungumzia barabara hii ya Chalinze mpaka Mlandizi, barabara hii ni ya muda mrefu na hata katika bajeti ya mwaka jana niliizungumzia, kwamba barabara ile imejengwa chini ya kiwango na pia hupelekea ajali nyingi hususan magari ya mizigo, na bado hapo katika hotuba ya Wizara Waziri anasema kwamba upembuzi yakinifu unaendelea kwa kilomita 12. 6.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini bado ipo haja, kwa umuhimu wa barabara hii nadhani ipi haja sasa, barabara hii ijengwe kwa kiwango ambacho ni madhubuti, itapelekea kutosababisha ajali katika barabara hii. Kwa sababu barabara hii ni kubwa, ya kupitisha magari ya kwenda Mikoa ya Kaskazini pia kwenda Mikoa ya Iringa, Mbeya na kwingineko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaona pia wakandarasi wetu, katika barabara kuu. Nitatolea mfano barabara ya Dodoma mpaka Morogoro, utakuta mkandarsi amepewa labda eneo la kukarabati, anachimba shimo, utakuta wiki tatu wiki mbili shimo lile halikarabatiwi na huweza kusababisha ajali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nashauri wakandarasi wetu pindi wanapopewa hii mikataba, watahadharishwe kwa sababu unakuta eneo wamechimba mashimo, wanataka wajenge na unakuta wiki mbili wiki tatu bado lile shimo halijazibwa na hii hupelekea kusababisha ajali kwa magari yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na pia ipo haja sasa ya kujua kwamba kwenye kitabu cha Waziri amesema kuanzia Morogoro mpaka hapa Dodoma ni kilomita 260 na upembuzi yakinifu unafanywa ili barabara hii ijengwe kwa kiwango, lakini sasa hivi naona kuna uakarabati unaendelea, hususan maeneo ya Dumila, barabara inatanuliwa, lakini sasa sijajua kama ndiyo imeingizwa kwenye hii bajeti au lile ni zoezi lingine linaendelea labda bajeti itakuja na barabara ile pia itabomolewa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kujua, pindi unapokuja hapa, lile zoezi linaloendelea maeneo ya Dumila pale, la kupanua barabara, lile linahusiana na huu upembuzi yakinifu unaoendelea? Maana yake naona ni vilaka vinazibwa, na eneo lile lina usumbufu wameweka mapipa barabarani na barabara yenyewe ni mbovu. Nataka nijue hawa wakandarasi wetu wanapopewa hii miradi, je, wanaelezewa kiwango cha upana wa barabara? Sidhani kama magari yetu sasa hivi yameongezeka ukubwa au upana, kwa sababu sasa hivi kinachoonekana ni barabara zinaongezwa upana. Kwa hiyo, nashauri Serikali, pindi mnapotoa tenda kwa wakandarasi wetu, muwaeleze upana halisi unaofaa katika barabara zetu za Tanzania, ili kuepusha upotevu wa fedha za Serikali katika kukarabati kila siku katika barabara hizi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ningependa kuelezea kuhusu reli, reli sasa hivi inajengwa reli hii ya mwendokasi, lakini bado kuna tatizo katika makutano ya pale Kamata. Ule ujenzi wa reli umepelekea sasa hivi kutokana na mvua za Dar es Salaam kuwa na mafuriko. Kwa hiyo, nilikuwa nashauri, yule mkandarasi aliyepo maeneo yale aweze kufanya jitihada za makusudi sasa kuweka miundombinu ambayo itawezesha sasa barabara ipitike kwa urahisi ambayo sasa hivi inaleta mafuriko kutokana na ujenzi unaoendelea, amezungusha mabati yake ambayo yanapelekea sasa hivi mafuriko katika eneo lile la Kamata. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ningependa kuelezea kuhusu reli yetu hii, reli inayojengwa ya mwendokasi watu wengi katika vijiji vyetu huwa wanaona kama ni jambo geni kwao, na ninashauri sasa hii reli inayojengwa sasa hivi ya kisasa ianze kuwekwa alama, mwisho ambao mwananchi anapaswa afanye shughuli zake. Kwa sababu isijeikatokea mwananchi sasa ameona reli imepita karibu na eneo analoishi, akaanza kuanza ujenzi ambao baadaye utapelekea sasa migogoro ya ardhi wakati sasa reli ilishakamilika na kukabidhiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba sasa wakati ujenzi unaendelea, alama ziwekwe katika hii reli ambayo inaanza ya mwendokasi, mpaka huku Makutupora, mpaka Kigoma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ningependa kuelezea kuhusu hii double parking, kuna maeneo mengi ambayo yako katika vituo, hizi barabara kubwa. Kwa mfano natolea mfano maeneo ya pale Kibaigwa, maroli makubwa yameweka double parking pande zote, kiasi kwamba yanasababisha magari ambayo yako katika mwendo anashindwa kupishana. Nashauri elimu itolewe kwa hawa wenye magari makubwa kwamba…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)