Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri Bima ya Afya iangalie utaratibu wa kupatia Bima Watanzania wote na bei ipungue.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia Hospitali ya Mrara inahitaji ujenzi wa wodi ya wazazi na watoto. Tunashukuru kwa mkopo wa Bima ya Afya milioni 108 kwa hospitali hiyo. Tunaomba mtuongezee kwani bajeti yake ni zaidi ya shilingi milioni 800.

Mheshimiwa Naibu Spika, Vituo vya Afya na Zahanati katika Kata zote za Babati Mjini vimejengwa na nguvu za wananchi, lakini hakuna fedha zozote za Serikali zimepelekwa kukamilisha maboma hayo. Tunaomba fedha za ukamilishaji maboma hayo ambayo ni Zahanati ya Singe, Sigimo, Mutuka, Himiti na Chemchem.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile tunaomba ambulance katika Hospitali ya Mrara.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawawatakia kila la heri katika majukumu yenu.