Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia hoja hii muhimu kwa mustakabali wa afya za wananchi wa Tarime. Kwanza niombe Wizara izingatie maoni yaliyotolewa na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, hasa maeneo ya Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971 kufanyiwa marekebisho ili kuweza kumlinda mtoto wa kike, maana ilivyo sasa inakinzana na sheria nyingine zinazomlinda mtoto.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili ni kuhusu hospitali yangu ya Mji wa Tarime ambayo ina hadhi ya kuwa Hospitali ya Mkoa wa Tarime/Rorya au kuifanya angalau hospitali ya wilaya. Tunakuwa treated kama vile hospitali inahudumia wananchi wa Tarime Mjini tu ilhali tunahudumia na wananchi wote toka Tarime Vijijini, Serengeti, baadhi ya maeneo ya Rorya na wengine wanatoka nchi jirani ya Kenya, lakini fedha tunazopokea za basket fund ni ndogo sana pamoja na stahiki nyingi za kuwezesha utolewaji wa huduma bora ya afya kama vile idadi ya Wauguzi/Wauguzi Wasaidizi inatolewa kwa idadi ya population ya Mji wa Tarime. Hii sio haki na inasababisha utolewaji wa huduma duni za afya na hatimaye kusababisha umauti.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna upungufu mkubwa wa Madaktari uliopelekea mosi na uchukuliwaji na ugawaji wa basket fund kwa kuzingatia idadi ndogo kuliko uhalisia; zoezi la vyeti feki; kustaafu na vifo. Tuna upungufu mkubwa sana. Wahudumu hawa, Madaktari wanafanya kazi kwa muda mrefu sana bila mapumziko na stahiki zao haziridhishi. Niiombe Serikali na juzi nilisema Bungeni kuwa tuna shida na Daktari wa Meno baada ya aliyekuwepo kufariki kwa ajali mwaka jana. Niombe sana suala hili lipewe kipaumbele maana sasa wananchi wanapata shida sana. Serikali ilichukulie kama jambo la dharura ili kuokoa afya ya kinywa na meno kwa wananchi wa Tarime.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba pia Wizara hii iweze kujenga utamaduni wa kutembelea magereza ili kujua manyanyaso wanayoyapata wanawake hawa wawapo kwenye mikono ya Jeshi la Polisi (vituoni), wengi wanabakwa na kudhalilishwa kijinsia. Pia waweze kuona ni jinsi gani wanawake maskini wanavyoonewa na kukosa misaada ya kisheria. Wengi wanakamatwa kwa makosa ya wanaume zao, wengine wana kesi za kudhaminika ila wapo, tena wengine wapo na watoto wadogo/wachanga, wengine ni mabinti wadogo sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kitendo cha Jeshi la Polisi kubaka/kuingilia kinyume wanawake tena mabinti ni kinyume kabisa na sheria na kanuni za kazi. Huu udhalilishaji ni lazima Wizara iufanyie kazi ili kulinda utu wa mwanamke.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni wakati sasa Serikali itenge fedha kwa ajili ya kitengo cha lishe. Serikali ya Awamu ya Tano haijawahi kutenga fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho ni mahitaji ya ambulance kwenye Kituo cha Afya cha Magena (Nkende) na kile cha Kenyamanyori. Upanuzi wa zahanati ile ya Nkongore Kenyamanyori na Ganasara (Nyandoto) kuwa Kituo cha Afya, ni muhimu sana na sisi tupate fedha za kukarabati na kupandisha hadhi ili ziweze kutoa huduma stahiki. Natambua huwa kuna fedha zinakuja tuweze kupatiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, cha kusikitisha mwaka huu wa fedha, yaani 2019/2020 hakuna bajeti ya uzazi na mpango (family planning). Ningependa kujua ni kwa nini hamna au ni kufuatia kauli ya Rais.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara lazima itoe elimu juu ya ugonjwa wa ini (hepatitis), magonjwa yasiyo ya kuambukizwa, kuwekeza kwenye kutoa elimu juu ya UKIMWI (HIV). Muhimu kuwekeza kwenye lishe, chanjo, vitamini kwa mama na watoto.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.