Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuwashukuru na kuwapongeza Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na wataalam wa afya kwa kazi nzuri zilizotukuka na kumuunga mkono wa dhati Rais Dkt. J.P. Magufuli na kuwezesha kuwa na matumaini ya kutimiza azma yake kwa akinamama na watoto hapa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunashukuru sana Mkoa wa Rukwa wamepatiwa pesa kwa ujenzi wa vituo vya afya na hospitali za wilaya zote nne na kuanza maandalizi ya awali ya ujenzi wa hospitali ya rufaa ya mkoa. Ombi letu ni Wizara ya Afya kutoa msukumo kwa TAMISEMI kuhakikisha wanaunga mkono jitihada na nguvu za wananchi katika kuyakamilisha maboma ya majengo ya zahanati yapatayo 50. Pia tunaomba vifaa tiba kwa wakati, ili zahanati takribani 15 zilizokamilika zipatiwe watumishi na zianze kazi kikamilifu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunashukuru kujengewa vituo vya afya vya kihistoria na bajeti ya 2019/2020 tumeongezewa vituo viwili ndani ya mkoa, ingawa bado mahitaji ni makubwa kwa Mkoa wa Rukwa kwani tupo pembezoni mwa nchi yetu (Congo DRC na Zambia). Tunaomba vifaa tiba na watumishi wa kukidhi mahitaji kwani majengo mazuri bila kuwa na hayo mahitaji hatutakuwa tumewafikishia wananchi huduma njema kwao.

Naomba Wizara kuona umuhimu wa Vituo vya Afya – Sopa, Kitete, Kala, Kabwe na kadhalika. Tuzingatie jiografia ya Rukwa ni mtihani kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na juhudi kwa hali halisi ya Waziri, bado Mkoa wa Rukwa tunaomba kuangaliwa kwa jicho la aina yake kwani, akinamama na vijana wameibuka katika kuinua uchumi wao kwa kujiunga kwenye vikundi vya ujasiriamali, tatizo lililopo ni elimu kwao, lakini Maafisa wa Maendeleo ya Jamii hawakidhi mahitaji. Si rahisi mmoja kushika vijiji viwili au mitaa sita au kata tatu, utendaji wao unakuwa hauna ufanisi na hata tija haipo. Tunaomba ajira itendeke kwa sasa, watumishi hawa ni muhimu sana vijijini, mitaani kwa afya, uchumi, maendeleo na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, maafisa hawa hawana usafiri. Tunaomba usafiri kwao na pikipiki kwa vijiji, mitaa na kata, magari kwa ngazi ya wilaya na mkoa kwani sasa inategemea huruma ya Mkurugenzi au RAS. Tunawarudisha nyuma kiufanisi kwao.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba upande wa Maafisa wa Maendeleo ya Jamii kuwa na ukaimu kwenye nafasi zao. Tunaomba eneo husika kuona kama vigezo vinakubalika waweze kupata nafasi hizo kikamilifu, ili wafanye kazi kwa tija na ufanisi uliotukuka kwa maslahi ya nchi yetu, hususan Mkoa wa Rukwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri wakati wa sherehe za Siku ya Wanawake Duniani, Mkoa wa Rukwa, alitoa ahadi ya kutoa ambulance ya Manispaa na Hospitali ya Mkoa, hivyo tunasubiri bado hizo ambulance mbili. Tunaomba Waziri aone namna ya kutimiza ahadi hii, kwani akinamama wanayumba sana kwa huduma hii ya usafiri.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunashukuru kwa hatua iliyofikiwa hadi sasa. Tunaomba kasi kuongezwa ili tufanane na mikoa iliyokamilishiwa kwa asilimia 50.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, tunaomba utaratibu wa Bima ya NHIF ukamilishwe haraka kwa kutolewa kwa wananchi wote kwa gharama nafuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.