Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru Mungu kwa kunipa afya njema na kuniwezesha kuchangia hoja hii. Pia napenda kuwapongeza kwa dhati Waziri na Naibu wake kwa kazi kubwa anazozifanya kwa kweli, wanajituma kwa nguvu zao zote kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya matibabu ya afya kwa kutupatia dawa na kupatikana vifaatiba katika hospitali zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, NHIF; huduma ya matumizi ya kadi ya bima ya afya NHIF tunahitaji watu wote wapate huduma hii ili wapate matibabu kwa kutumia huduma hii kwa urahisi, lakini bado tuko nyuma, mpaka sasa wanaotumia huduma hii ni asilimia 34 tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Watanzania wanataka elimu ya kutosha itolewe hasa vijijini, ili wapate uelewa juu ya matumizi ya bima ya afya na vievile waweze kutibiwa kwa daraja lake ili yule mwenye maisha duni aweze kutibiwa kwa uwezo wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu viongozi wanaotumia huduma hii mfano Wabunge, wanatibiwa yeye pamoja na mwenza wake na watoto wanne, lakini mzazi wake hapati huduma hii. Swali langu ni hili je, hatuoni Serikali haijawatendea haki wazee kuwakosesha huduma hii?

Mheshimiwa Naibu Spika, sina budi kuipongeza Serikali kwa Taasisi ya Moyo kuweza kutupatia tiba na wataalam mbalimbali kuhusu tatizo hilo. Tunaomba tiba hii ipatikane katika hospitali nyingine za rufaa mbalimbali katika nchi yetu, ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Muhimbili.

Mheshimiwa Naibu Spika, Madaktari na Wauguzi pamoja na wafanyakazi mbalimbali wa sekta ya afya. Hawa wote wanafanya kazi katika mazingira magumu kutokana na kazi zao. Kwanza tunaomba waangaliwe, maslahi yao yaboreshwe ili waweze kupata ari na upendo wa kazi yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Madaktari, Wauguzi na Nesi wana changamoto mbalimbali zikiwemo posho ya nyumba, motisha ya saa za ziada. Hili tatizo kubwa linaweza kuathiri utendaji kazi wao, kwa hiyo, naiomba Serikali iliangalie tatizo hili kwani hawa ndio wanaotuokoa katika maisha yetu ya kila siku.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu vifo vya wajawazito bado ni changamoto katika nchi yetu, baada ya kupungua bado vinaongezeka katika Taifa letu. Kwanza naipongeza Serikali kupitia Wizara ya Afya, juzi nilishuhudia kwenye vyombo vya habari kuwa inatoa michango mbali ya fedha kutaka kuwasajili Wakunga wa Jadi ili kuweza kusaidia kupunguza vifo vya akinamama wajawazito na watoto. Ahsante sana Waziri Ummy, wanawake tunaweza.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya mchango wangu, naunga mkono hoja.