Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Muhammed Amour Muhammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Bumbwini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote ni vyema nikamshukuru Mwenyezi Mungu wa rehema kwa kunipatia afya njema na busara ya kuweza kuchangia mada iliyopo hapa mezani. Pia, nikushukuru kwa kunipa fursa nami niweze kuchangia hoja hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa homa ya matumbo ya kuendesha, imekuwa ni tabia ya kawaida kila baada ya miongo ya mvua hutokea maradhi ya milipuko ya matumbo. Ni vyema Serikali ingefikiria zaidi namna ya kuwalinda wananchi wetu ili kuzuia maafa haya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu masuala ya maambukizi ya UKIMWI, ni hali yenye kutisha, mazingira ya kupambana na UKIMWI hayajaridhisha kabisa, bado vijana wetu hawajakuwa na hadhari ya kutosha na maambukizi bado yanaendelea kutisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, niende sasa kuhusiana na maradhi yasiyo ya kuambukizwa. Kumekuwa na hadhari kubwa kuwaeleza wananchi kufanya mazoezi na timu mbalimbali zimeanzishwa ili kukidhi haya mahitaji lakini je, Serikali ina mkakati gani mahususi wa kulisimamia hili na kulipigia debe kwa wananchi wote hasa vijijini?

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niende kwenye medical instruments kama ct-scan, ultra sounds, x-rays tube. Hivi vyombo ni muhimu na ni bado havijaenea nchini, bado vijijini hizi zana hazijafika. Niombe sana Serikali kwa namna ya pekee ieneze hizi zana kwa haraka sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.