Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Njombe ni miongoni mwa mikoa inayojengewa Hospitali za Rufaa. Hospitali ya Mkoa wa Njombe imewekwa jiwe la msingi na Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Waziri katika maelezo yake kabla kuwekewa jiwe la msingi mbele ya Mheshimiwa Rais na mbele ya umati wa wananchi wa Njombe Mjini, aliahidi hospitali yetu itaanza kazi mwezi Julai na maelezo hayo yalirudiwa tena wakati wa kumkaribisha Mheshimiwa Rais kuweka jiwe la msingi. Wananchi wa Njombe tungefurahi sana kuona Hospitali yetu mpya inaanza kutoa huduma kama alivyoahidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jambo ambalo linanitia shaka wakati Mheshimiwa Waziri akiwasilisha bajeti yake hajaonesha bayana kama hospitali hii itafunguliwa kama alivyoahidi. Nimepitia Kitabu cha Hotuba sijaona kabisa fungu mahususi kwa vifaa vya hospitali vipya. Naomba wakati wa kuhitimisha hotuba, Mheshimiwa Waziri atoe kauli ya Serikali ndani ya Bunge kututhibitishia wananchi wa Mkoa wa Njombe kuwa hospitali yetu itaanza kutoa huduma kama alivyotuahidi. Vinginevyo namfahamisha mapema Mheshimiwa Waziri kwamba nitazuia shilingi ya mshahara wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.