Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja ya Waziri, lakini pia naipongeza Wizara yote kwa ujumla kwa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi pamoja na changamoto ya ufinyu wa Bajeti (fedha) zinazowakabili.

Mheshimiwa Naibu Spika, huduma za kinga hususan chanjo ni muhimu sana katika suala la afya za watoto miaka walio na umri wa chini ya miaka mitano na wanawake wajawazito. Ili Wizara iweze kutekeleza kwa ukamilifu huduma hii inahitaji uwepo wa dawa, chanjo na vifaa vya kutolea chanjo pamoja na usafiri.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Malinyi inatekeleza huduma za chanjo kwa ugumu sana kwa kutokuwepo na gari la chanjo. Kubwa zaidi wilaya inakabiliwa na uhaba mkubwa na magari, hivyo kusababisha Idara yote ya Afya katika Wilaya ya Malinyi haina kabisa gari la kuhudumia shughuli za afya ikiwemo huduma za utoaji chanjo.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kutokuwepo na gari la chanjo au gari maalum kwa huduma za afya katika Wilaya ya Malinyi; nimemtaarifu Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalimu naye aliahidi kutupatia gari moja zitakapowasili gari maalum za chanjo mwishoni kwa 2018. Gari hizo za chanjo zimefika, lakini Wilaya ya Malinyi haijatengewa gari hata moja, tunaomba gari moja toka Wizara ya Afya kwa huduma za afya katika Wilaya ya Malinyi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.