Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, pongezi kwa Serikali kwa kutujengea Kituo cha Afya Malangali, Kata ya Malangali ambacho kitatoa huduma katika Kata tatu za Ihwanza, Idunda na Malangali yenyewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, pongezi pia kwa kutujengea Hospitali ya Halmashauri ya Mufindi ambayo itahudumia kata 27 katika Wilaya ya Mufindi pia itatoa huduma kwa watu wote ndani na nje ya Watanzania sababu ni Halmashauri yenye wafanyakazi wengi sana na wawekezaji wengi wakubwa na wadogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali kumalizia Kituo cha Afya cha Kata ya Mtwango na Kituo cha Afya cha Kata ya Mninga. Serikali imalizie ujenzi wa Zahanati katika Kijiji cha Nzivi, Kinegembasi, Iramba, Nyigo, Udumka na Ikaning’ombe.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia Serikali ituletee Watumishi katika vituo vyetu tuna tatizo kubwa la watumishi katika Jimbo la Mufindi Kusini. Nitashukuru sana kama Serikali itatekeleza kwa muda maombi hayo.

Ahsante na naunga mkono hoja.