Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Waziri wa Wizara hii, Mheshimiwa Dkt. Faustine Ndugulile, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote kwa hotuba nzuri yenye uelewa, pia kwa kazi nzuri wanayofanya kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nishukuru sana kwa ongezeko la madawa na vifaa tiba. Ushauri; kwa kuwa Hospitali ya Rufaa Kitete ina majengo ambayo hayajakamilika, niombe Serikali ikamilishe ili yaweze kutumika hasa Chuo cha Uuguzi. Nishauri pia katika majengo yanayojengwa sasa ni vema yakazingatia ujenzi na jengo la mama Ngojea, ili wanawake wengi waweze kupumzika wanaposubiri kujifungua, ishirikiane na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Wizara kutenga sehemu maalum katika kila Kituo cha Afya kwa ajili ya kutunzia watoto Njiti.

Mheshimiwa Naibu Spika, magonjwa; niombe elimu iendelee kutolewa kwa ajili ya ugonjwa wa dengue, Ini, ili wananchi wengi waweze kujua tiba yake, tahadhari pia. Kwa nini ugonjwa huu wa dengue haupo kwenye Bima za Afya? Kwani wananchi wengi wanasumbuka.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile naomba Serikali ipeleke mashine za kupimia sukari katika Vituo vya Afya na Zahanati ili kuokoa maisha ya wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Benki ya Wanawake; kwa kuwa benki hii tangu ianze haijatoa gawio lolote mpaka sasa na mimi nikiwa ni mhanga wa kutoa hisa (hisa Milioni mbili) nini hatima yangu? Kwa kuwa fedha yangu imekaa muda mrefu, je, naruhusiwa kuuza hisa zangu, ili niipate fedha yangu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia Benki ya Wanawake lini itafika Mkoa wa Tabora ili wanawake waweze kukopa. Niombe Serikali iweke Dirisha la ukopaji kwenye Benki ya TPB.

Mheshimiwa Naibu Spika, usafi wa mazingira, kwa kuwa maeneo mengi hususan Hospitali ya Rufaa Kitete kuna vifaa chakavu kama vile vitanda, meza na magari, je, hakuna utaratibu wa kuuza au kuviondoa kwenye eneo la hospitali na kupeleka eneo lingine? Kwa kuwa vinawekwa eneo la nje na kusababisha mazalia ya mbu. Niombe Wizara itembelee hospitali yangu na kuona hali halisi (Kitete Tabora).

Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971; niishauri Serikali kuleta haraka Sheria ya Mabadiliko ya Sheria Ndoa ili wanawake na watoto wapewe haki zao. Ukatili wa kijinsia unaongezeka hapa nchini, kunyimwa haki wajane na kudhulumiwa mali zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono.