Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, niwapongeze Mheshimiwa Waziri Ummy Mwalimu pamoja na Naibu Waziri, Mheshimiwa Dkt. Faustine Ndugulile kwa kazi nzuri wanazozifanya katika Wizara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali fedha zinazopitishwa katika bajeti zifikishwe kwa wakati ili majukumu yaliyopangwa yaweze kutekelezwa kwa wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, kipimo cha Dengue ni ghali sana kwa wananchi wenye kipato cha chini. Mfano katika Hospitali ya Temeke ni Sh.40,000 na Regency Hospitali ni Sh.77,000 na hata kama una Bima ya NHIF ya Bunge unalipia cash hususan Regency Hospitali. Nashauri kutokana na ugonjwa huu kuwa katika Mikoa ya Pwani, Tanga, Dar es Salaam na kadhalika na kipindi hiki cha mvua watu wengi huugua na kushindwa kupata fedha za kulipia kipimo cha Dengue, Serikali ipunguze gharama za upimaji wa ugonjwa huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Rufaa Temeke Dar es Salaam, eneo lake ni dogo na wodi nyingi ni chakavu na hazikidhi mahitaji ya wagonjwa. Nashauri zile wodi za zamani zibomolewe yajengwe maghorofa. Mfano mzuri Regency Hospitali Dar es Salaam eneo lilikuwa dogo likabomolewa wakajenga maghorofa ili kukidhi mahitaji wagonjwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Rufaa Muhimbili na Mloganzila Dar es Salaam. Naishauri Serikali ijenge jengo la kusubiria wagonjwa kwa wale ndugu na jamaa wanaowasindikiza wagonjwa wao watokao Mikoani ili waweze kutoa msaada wa kijamii kwa wagonjwa wao maana siyo wagonjwa wote wana ndugu katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali itoe elimu ya kutosha kwa wale wananchi wanaonunua miwani hovyo bila kupimwa iwe kwa ajili ya urembo au la, wasivae bila kupewa ushauri kutoka kwa madaktari wa macho. Maana kuna baadhi ya wananchi wamepata matatizo ya macho kwa kununua miwani bila kufuata ushauri wa daktari.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka jana nilitoa ushauri Serikali iondoe tozo katika maiti hususani katika hospitali zetu zote. Maana ni kero kwa wafiwa na wakati mwingine walimuuguza ndugu yao kwa kipindi kirefu na walitumia gharama nyingi sana na marehemu wakati wa uhai wake alikuwa na mlipa kodi mzuri kwa kununua bidhaa mbalimbali kwa mahitaji ya kila siku. Hivyo, naishauri Serikali iondoe tozo/ malipo kwa maiti katika hospitali zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na matangazo mengi haswa Dar es Salaam ya Waganga wa Jadi na vipeperushi vingi hugaiwa katika makutano ya barabara. Naishauri Serikali hawa Waganga wa Jadi watoe matangazo yao katika vyombo husika kama redio, televisheni na magazeti na siyo kubandika katika nguzo za umeme, miti na kutoa vipeperushi barabarani.