Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Tabora Kaskazini lina kituo kimoja tu cha afya. Namwomba sana Waziri tuipandishe hadhi Zahanati ya Ilolangulu iwe kituo cha afya ili kwa jumla tuwe na vituo viwili vya afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Waziri na Naibu Waziri kwa kazi nzuri wanayofanya, hongereni sana. Pia nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kuwajali wanyonge, Wilaya ya Uyui tumepewa Hospitali ya Wilaya inayojengwa kwa shilingi bilioni 1.5 pia Kituo cha Afya cha Upuge kwa shilingi milioni 500. Namkaribisha Mheshimiwa Waziri atembelee Jimbo langu na Kituo cha Afya cha Upuge lakini pia Zahanati ya Ilolangulu ili ajionee mwenyewe ujenzi uliofanyika hasa katika zahanati na akiridhia kiwe kituo cha afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, naomba gari la wagonjwa (ambulance) kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Upuge.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.